Cheki picha 6 za Mali zilizoteketea kwa kosa la kuchoma moto kituo cha polisi cha Mugoma wilayani Ngara mkoani Kagera na kusababisha hasara yenye thamani ya zaidi shilingi milioni 68. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Monday, December 24, 2012

Cheki picha 6 za Mali zilizoteketea kwa kosa la kuchoma moto kituo cha polisi cha Mugoma wilayani Ngara mkoani Kagera na kusababisha hasara yenye thamani ya zaidi shilingi milioni 68.

Mali zilizoteketea kwa kosa la kuchoma moto kituo cha polisi cha Mugoma wilayani Ngara mkoani Kagera  na kusababisha hasara yenye thamani ya zaidi shilingi milioni 68, kutokana na uharibifu wa mali mbalimbali za jeshi hilo.




Hadi sasa tayari wakazi sita wa kijiji cha Mugoma wilayani Ngara, wamefikishwa katika Mahakama ya wilaya ya Ngara mkoani Kagera  wakishitakiwa kwa mauaji ya Askari wawili na kuchoma moto kituo hicho cha Polisi kata ya Mugoma wilayani humo.


 

Kwa mujibu wa waendesha mashitaka wa Jeshi la Polisi Hamisa Mataka na Tumaini Membi, wamewataja washitakiwa kuwa ni Method John  ambaye ni afisa Mtendaji wa kijiji cha Mugoma, Suleimu Zuberi, Rashid Ally, Issa Athumani, Simon Chuma na Aman Maulid.



Washitakiwa hao wanatuhumiwa kuwaua Koplo Paschal na Konstebo Alexandar, ambao walikuwa waajiriwa wa jeshi la polisi Tanzania, katika tukio lililotokea Desemba 15 mwaka huu huku  Katika shitaka la pili, watu hao wanashitakiwa kwa kosa la kuchoma moto kituo cha polisi cha Mugoma, na kusababisha hasara yenye thamani ya zaidi shilingi milioni 68, kutokana na uharibifu wa mali mbalimbali za jeshi hilo.



Washitakiwa wako  rumande hadi January 3 mwaka 2013 kesi hiyo itapkapotajwa tena.





Picha na :Wiliam Mpanju.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad