Siku chache
baada ya kukamilisha kushoot video ya ngoma yake
mpya ya 'Sorry' nyota kutoka nyumba ya vipaji nchini (THT) Barnaba Boy amesema
ni upumbavu kwa wasanii wa muziki wa kizazi kipya nchini kushoot video za
muziki wao kutoka maeneo ya nje ya nchi.
Katika
mahojiano maalum aliyoyafanya na teentz.com mapema leo Barnaba amesema kuwa,
wakati mwingine inaweza isiwe jambo baya lakini
kwake anaona ni upumbavu kufanya hivyo wakati nchi hii ya Tanzania imebarikiwa kuwa na vitu kibao vya kuvutia
ambavyo vinaweza kupamba video ya wimbo husika.
"Hivi
sasa naona watu wengi wanakimbilia kufanya video nje, si mbaya lakini binafsi
siwezi fanya jambo hilo kwa kuwa naipenda nchi yangu na natamani kuendelea
kuitangaza kila siku soo nahisi ni jambo bora kufanya video zangu hapa,bongo
kwa kutumia warembo wa hapa na huo ndiyo uamuzi wangu ambao nahisi
sitaubadilisha kamwe" alisema.
No comments:
Post a Comment