Mabingwa wa Ulaya Chelsea yawadunda Norwich bao 4 – 1 na kujiimarisha kileleni mwa Ligi Kuu ya Uingereza. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Saturday, October 06, 2012

Mabingwa wa Ulaya Chelsea yawadunda Norwich bao 4 – 1 na kujiimarisha kileleni mwa Ligi Kuu ya Uingereza.



Mabingwa wa Ulaya Chelsea imejiimarisha kileleni mwa Ligi Kuu ya Uingereza  baada ya kuichapa mabao 4-1 timu ya  Norwich  wakiwa nyumabani darajani Stamford Bridge. 


Grant Holt aliifungia Norwich bao la kuongoza dakika ya 11, lakini Chelsea ilisawazisha kupitia kwa Fernando Torres kabla ya Frank Lapard na Eden Hazard kufunga mabao ya ushindi kipindi hicho hicho cha kwanza na Branislav Ivanovic kuhitimisha karamu ya mabao ya ushindi wa 4-1 zikiwa zimebaki dakika 15.


Chelsea imefikisha pointi 19, baada ya kucheza mechi saba na kuendelea kuongoza Ligi Kuu  ikiwazidi pointi nne mabingwa watetezi, Man City  ambao nao wameshinda bao 3 - 0     dhidi ya Sunderland kwa magoli ya  Kolarov (4), Aguero (59) na  Milner (88).  



Aidha matokeo mengine ya Ligi hiyo soka Uingereza ni 


West Brom          3 - 2  QPR

Swansea    2 - 2  Reading

Wigan         2 - 2  Everton

Jumapili Oktoba 7

[Saa 9 na Nusu Mchana]

Southampton v Fulham


[Saa 11 Jioni]

Tottenham Hotspur v Aston Villa

Liverpool v Stoke City

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad