Mabingwa Hispania waendelea kutesa juu katika Viwango vya FIFA VYA UBORA WA SOKA Duniani huku Tanzania kuganda pale pale nafasi ya 132. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Wednesday, October 03, 2012

Mabingwa Hispania waendelea kutesa juu katika Viwango vya FIFA VYA UBORA WA SOKA Duniani huku Tanzania kuganda pale pale nafasi ya 132.

Mabingwa wa Ulaya na Dunia, timu ya taifa ya Hispania wameendelea kushika nafasi ya kwanza kwenye Listi ya viwango bora vya soka Duniani vya  FIFA/Coca Cola viliyotolewa leo huku timu ya taifa ya Tanzania ikibakia nafasi ya 132 kwenye ubora huo huku  kwenye Kumi Bora ,Timu ya taifa ya Ureno ikipanda na kushika namba 3, Uingereza ikiporomoka na sasa ipo nafasi ya 5 kutoka nafasi ya  3 mwezi uliopita.




Barani Afrika Tembo wa Africa ,Ivory Coast ndiyo wapo juu na wapo nafasi ya 16 ambayo ni ile ile kama ilivyokuwa Mwezi uliopita.


Timu ya taifa ya Colombia wameingia Kumi Bora baada ya kupanda nafasi 13 huku Denmark na Croatia zikiporomoka kutoka Kumi Bora.


Aidha Brazil ambao ni mabingwa wa Dunia mara 5, wameporomoka nafasi mbili na sasa wapo nafasi ya 14.


KUMI NA TANO  BORA FIFA/COCA COLA:

1 Spain

2 Germany

3 Portugal

4 Argentina

5 England

6 Netherlands

7 Uruguay

8 Italy

9 Colombia

10 Greece

11 Croatia

12 Russia

13 France

14 Brazil

15 Switzerland

Listi nyingine mpya itatolewa Novemba 7.





No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad