![]() |
Leo Arsenal wakiwa ugenini huko Anfield wameipiga Liverpool Bao 2-0 kwa bao za wachezaji wao Lukas Podolski na Santi Cazorla ambazo zimewaacha Liverpool wakiwa hawajashinda hata Mechi moja ya Ligi Msimu huu baada ya Mechi 3.
Arsenal walipata bao la kwanza katika Dakika ya 31 pale Nahodha wa Liverpool Steven Gerrard alipotaka kupenyeza pasi kwa Luis Suarez akiwa karibu na boksi la Arsenal lakini pasi hiyo ilinaswa na Arsenal na Arsenal wakawa wako mbele kwa bao moja baada ya mpira huo kupewa Santi Cazorla aliechomoka nao na kumpa pande Lukas Podolski ambae shuti lake la chini lilimshinda Kipa Pepe Reina.
![]() | ||
| Bao la pili la Arsenal lilifungwa katika ya Dakika ya 68 kwa shuti kali la Santi Cazorla na safari hii alikuwa Lukas Podolski aliempa pasi Santi Cazorla. |
Tottenham wakicheza kwao White Hart Lane wameendelea kupata matokeo ambayo si mazuri kwao kufuatia sare ya bao 1-1 na Norwich City hii ikiwa ni sare ya pili baada ya kufungwa Mechi ya kwanza ya Ligi Kuu Uingereza.
Spurs walipata bao lao mfungaji akiwa Mchezaji wao mpya Moussa Dembele akicheza Mechi yake ya kwanza kabisa na alifunga bao hilo zuri katika Dakika ya 69.
Norwich walisawazisha katika Dakika ya 85 kwa bao la Robert Snodgrass.
Tottenham walijikuta wakiwa Mtu 10 katika Dakika ya 90 baada ya Kiungo wao Tom Huddlestone kupewa Kadi Nyekundu kwa kile kilichoonekana ni rafu mbaya na Refa Mark Halsey lakini huenda hii ikafutwa akikata Rufaa.
![]() |
|
Michezo ya muda huu
ni: Southampton 2 v 1 Manchester United Newcastle United 0 v 1 Aston Villa Na matokeo unaweza kutazama kwa juu katika blogge hii. |











No comments:
Post a Comment