![]() |
|
|
Timu ya
Taifa ya Hispania ambao ndio Mabingwa wa
Ulaya na Dunia, wameendelea kushika nafasi ya kwanza kwenye Listi ya FIFA/Coca Cola ya Ubora
Duniani iliyotolewa leo (September 5) huku Tanzania ikiporomoka nafasi 4 na
kushika nafasi ya 132 lakini kwenye Kumi
Bora hamna mabadiliko yeyote isopokuwa Ureno
kupanda nafasi moja na kushika nafasi ya 4 huku Uruguay ikishuka nafasi
moja na kukamata ya 5.
Hispania,
Ujerumani na Uingereza zimeendelea
kung’ang’ania nafasi za kwanza, pili na tatu kama ilivyokuwa Julai mwaka huu,
ambapo Hispania ina pointi 1617, Ujerumani 1437 na England 1274.
Brazil,
Mabingwa wa Dunia mara 5, wamepanda nafasi moja na sasa wapo nafasi ya 12 na kushindwa
kurejea katika 10 bora, ambako imetoka nafasi ya 13 hadi 12 ikiwa na pointi
996, huku mahasimu wao Argentina wakibaki nafasi ya saba kwa pointi 1121.
Kwa Afrika,
Timu ambayo iko juu kabisa ni Ivory Coast iliyobaki nafasi yake ile ile ya 16 na wanaongoza Bara la Afrika, ambapo kidunia imeendelea kushikilia nafasi ya 16
kwa mwezi wa pili mfululizo ikiwa na alama 912, huku Algeria ikiipindua Ghana
baada ya kupanda kwa nafasi sita kutoka 34 hadi 28, huku Ghana ikipanda kwa
nafasi moja hadi 31.
Aidha
Tanzania imeporomoka kwa nafasi nne katika viwango vya ubora wa soka duniani
vya Agosti 2012 vilivyotolewa na Shirikisho la Soka la Kimataifa (FIFA) jana.
Wakati
viwango vya Julai vilionesha Tanzania kuwa nafasi ya 128, vipya vimeishusha
hadi 132, ikijikusanyia pointi 243, ambapo katika mwezi huo, ilicheza mechi
mbili na kwenda sare ya mabao 3-3 na Botswana Agosti 15 jijini Gaborone na ile
ya 1-1 dhidi ya Ghana.
Kwa mujibu
wa viwango hivyo, majirani Uganda wamebaki katika nafasi yao ya 88 wakiwa na
ponti 401 huku Kenya ikipanda kwa nafasi
moja kutoka 126 hadi 125, wakiwa na pointi 268.
Mabingwa wa
Afrika, Zambia, wamejikongoja taratibu, wakipanda kwa nafasi mbili kutoka 44
hadi 42, wakiwa na alama zao 624.
Listi nyingine mpya itatolewa Oktoba
3
KUMI BORA:
[Kwenye Mabano nafasi za Mwezi
uliopita]
1. (1) Hispania
2. (2) Ujerumani
3. (3) Uingereza
4. (5) Ureno
5. (4) Uruguay
6. (6) Italia
7. (7) Argentina
8. (8) Uholanzi
9. (9) Croatia
10. (10) Denmark
Viwango vya timu nyingine za Taifa
ingia hapa http://www.fifa.com/worldranking/rankingtable
ili kuvitazama.







No comments:
Post a Comment