Na Shaaban Ndyamukama Ngara.
Miradi 10 yenye thamani ya
shilingi milioni 635 laki 8 na 17,000 katika Halmashauri ya wilaya ya Ngara
mkoani Kagera inatarajiwa kupitiwa na mbio za mwenge utakaowasili septemba 7
wilayani humo .
Akiongea na waandishi wa habari ofisini kwake jumatatu wiki hii Kaimu
mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Ngara Simon Mumbee amesema kamati ya mwenge ya mkoani Kagera ilipitisha
miradi hiyo 10 kati ya miradi 14 iliyokuwa imependekezwa na kamati ya mwenge wilayani Ngara .
Mumbee alisema kuwa miradi
hiyo itafunguliwa ,kukaguliwa ,kuzinduliwa na kuwekewa mawe ya msigi
katika kata za Rusumo , kasulo, Rulenge
Keza na mwenge utakesha katika kata ya
Murusagamba na kesho yake utakabidhiwakatika
kijiji cha Nyabibuye wilaya mpya ya Kakonko mkoani Kigoma.
Alisema kuwa katika miradi
hiyo serikali kuu ilichangia shilingi zaidi ya milioni 400 wananchi walichangia shilingi milioni 150 na
fedha nyingine ilichangiwa na Halmashauri pamoja na wahisani mbalimbali
wilayani humo.
|
Wakimbiza Mwenge kitaifa na
baadhi ya makamanda wa jeshi la polisi wakishuka baada ya kuwasha mwenge wa
Mwitongo.
|
Naye martibu wa mbio za
mwenge wilayani Ngara Bakari Salumu alisema mwenge utaweka jiwe la msingi katika ujenzi wa shule ya
sekondari Rusumo Maporomoko, mradi wa maji Kafua kata ya Kasulo, ujenzi wa kituo cha polisi cha kata ya
keza na mradi wa barara ya Murubanga hadi
Mursagamba kuelekea mpakani na nchi jirani ya Burundi.
Bakari alisema katika pia
mwenge utafungua mradi wa eneo la mnada lililoko Benako, kufungua josho la
mifugo Kumubuga kata ya Rusumo na ujenzi wa Zahanati ya Magamba .
Aidha alisema kuwa katika
uzinduzi mwenge utazindua bwalo la shule ya sekondari ya RHEC Rulenge na
kukagua shamba la miti la mtu binafsi kata ya Murusagamba ambapo aliwataka
wananchi kujitokeza kuupokea mwenge huo ulio na kauli mbiu ya shiriki sensa , toa maoni katika
mchakato wa katiba mpya na jihadhari na VVU pamoja na kupinga vikali vitendo
vya rushwa.





No comments:
Post a Comment