Ligi Kuu Bara, rasmi kama Vodacom Premier League inayoanza leo Jumamosi (September 15) Bingwa mwaka huu anapata Shilingi 70 milioni ambazo ni sawa na mshahara wa mwaka mzima wa straika wa Simba, Mzambia Felix Sunzu. . - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Saturday, September 15, 2012

Ligi Kuu Bara, rasmi kama Vodacom Premier League inayoanza leo Jumamosi (September 15) Bingwa mwaka huu anapata Shilingi 70 milioni ambazo ni sawa na mshahara wa mwaka mzima wa straika wa Simba, Mzambia Felix Sunzu. .

Felix Sunzu
Bingwa  wa Ligi Kuu Bara inayoanza leo Jumamosi (September 15)mwaka huu anapata Shilingi 70 milioni ambazo ni sawa na mshahara wa mwaka mzima wa straika wa Simba, Mzambia Felix Sunzu.



Kampuni ya Simu za Mkononi ya Vodacom imeingia mkataba wa miaka mitatu na Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) wa kudhamini ligi hiyo ikiwa imepanga kutumia kiasi cha Sh 1.7 bilioni.


Mshindi wa pili wa ligi hiyo atajizolea, Sh 50 milioni wakati Sh 30 milioni zitakwenda kwa mshindi wa tatu.


Sunzu analipwa Dola 3,500 kwa mwezi ambazo ni sawa na Sh 5.4 milioni ambazo ukizidisha kwa miezi 12 anapata Sh 65.1 milioni na ukiongeza na posho za mechi na gharama ndogondogo ambazo klabu inaingia, zinazidi Sh 70 milioni za bingwa wa ligi.


Klabu zimekuwa zikilalamikia ufinyu wa zawadi huku TFF ikitangaza kwamba mkataba mpya na mdhamini umeshasainiwa ingawa hakuna picha zozote za ushahidi zilizoonyesha wahusika wakianguka wino.



Ligi Kuu inashirikisha timu 14 ambazo zitacheza mechi 26 kuzunguka mikoa mbalimbali kila timu ikiwa na usajili wa wachezaji wasiopungua 25.


Huku udhamini wa Tanzania ukiwa kiduchu huko Afrika Kusini ambako kampuni za huko zimewekeza Tanzania katika sekta za madini, fedha na mawasiliano zinatoa zawadi za kufa mtu.


Mathalan bingwa wa Ligi Kuu Afrika Kusini inayodhaminiwa na Benki ya ABSA, ambayo ina hisa kubwa katika Benki ya Biashara ya Tanzania (NBC), bingwa anaondoka na kiasi cha Sh 1.9 bilioni.


Mshindi wa pili wa ligi hiyo anaondoka na kiasi cha Sh 926 milioni huku mshindi wa tatu akiweka kibindoni Sh 370 milioni.


Kinachoshangaza ni kuwa kampuni za kigeni zilizowekeza nchini zinamwaga mamilioni huko makwao lakini linapokuja suala la kudhamini michezo ya Tanzania, zinatoa zawadi ndogo wakati wanafaidi rasilimali mbalimbali kupitia uwekezaji wao.


Aidha Ligi kuu Tanzania Bara ambayo katika misimu mitano iliyopita hakuna mfungaji bora aliyewahi kufikisha mabao 20, inaanza leo Jumamosi huku kazi kubwa ikiwa kwa vinara watatu Simba, Yanga na Azam.


Msimu huu ambao Simba ni mabingwa watetezi kuna timu 14 huku miji yote mikubwa ya Tanzania ambayo ni Arusha, Tanga, Dar es Salaam, Mwanza na Mbeya yakiwa na timu.


Simba itacheza na African Lyon kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam, huku Polisi Morogoro na Mtibwa Sugar zikicheza Uwanja wa Manungu, Yanga itakuwa Mbeya kwa Prisons kwenye Uwanja wa Sokoine, huku watani wa jadi JKT Mgambo na Coastal Union wakipambana katika Uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga.


imeandikwa na:http://www.mwanaspoti.co.tz.


No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad