![]() |
| Robin van Persi |
Man United walianza vibaya katika Mechi hii pale udhaifu wa Difensi yao , ambayo Kiungo Michael Carrick kwa mara ya pili akicheza kama Sentahafu, ilipofanya makosa na kuwapa Fulham bao la kwanza katika Dakika ya 3 tu.
Lakini bao za Robin van Persi, Shinji Kagawa na Rafael ziliwafanya Man United wawe mbele kwa bao 3-1 hadi mapumziko.
Udhaifu wa Difensi ya Man United uliwapa zawadi bao la pili Fulham pale Vidic na Kipa De Gea walipocheza ovyo na Vidic kujifunga mwenyewe.
![]() |
| Chelsea |
Nao Mabingwa wa Ulaya Chelsea wakicheza Mechi yao ya tatu za Ligi Kuu Uingereza, kila Mechi wakipata na kufunga Penati, sasa wameshinda Mechi zote hizo tatu na wako kileleni, ambapo wakicheza kwao Stamford Bridge wameichapa Newcastle bao 2-0.
Chelsea walipata bao lao la kwanza katika Dakika ya 22 kwa Penati iliyopigwa na Mchezaji wao mpya Eden Hazard na bao lao la pili katika Dakika ya 45 kwa bao la Fernando Torres baada ya kutengenezewa na Eden Hazard.
Mechi inayofuata kwa Chelsea ni huko Monaco hapo Agosti 31 kugombea UEFA Super Cup dhidi ya Atletico Madrid ambao ni Mabingwa wa EUROPA LIGI.
![]() |
| Brendan Rodgers |
Liverpool wako kwao Anfield na watataka ushindi baada ya kutwangwa 3-0katika Mechi yao ya kwanza ya Ligi mikononi mwa WBA lakini, hata hivyo, watamkosa Sentahafu wao Daniel Agger ambae alitolewa kwa Kadi Nyekundu katika kipigo hicho Wikiendi iliyopita.
![]() |
| Nasri na Toure |
![]() |
| Arsene Wenger |
Stoke wanategemewa kumuanzisha Mchezaji mpya Geoff Cameron ambae atacheza Kiungo pamoja na Glenn Whelan huku Jonathan Walters akicheza nyuma tu ya Straika Peter Crouch.
![]() |
| Lukas Podolski |
Kwa Arsenal, Santi Cazorla, Mikel Arteta na Abou Diaby wataendelea kucheza Kiungo baada ya kucheza vizuri katika sare na Sunderland huku Fowadi ikikamatwa tena na Gervinho na Lukas Podolski.
Arsenal wana nafasi nzuri kushinda Mechi hii lakini inabidi waidhibiti nguvu kazi ya Stoke City.
Aidha kwa Matokeo na ratiba za Ligi nyingine unaweza tazama LIVE kwenye Blogg hii kwa juu.












No comments:
Post a Comment