Leo Agosti 26, 2012 Viongozi mbalimbali nchini Tanzania walipojiunga na mamilioni ya Watanzania katika zoezi la sense ya watu na makazi lililofanyika kwa mafanikio makubwa nchi nzima na litadumu kwa muda wa siku saba. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Sunday, August 26, 2012

Leo Agosti 26, 2012 Viongozi mbalimbali nchini Tanzania walipojiunga na mamilioni ya Watanzania katika zoezi la sense ya watu na makazi lililofanyika kwa mafanikio makubwa nchi nzima na litadumu kwa muda wa siku saba.


Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwa na mkewe Mama Salma Kikwete na familia yake akijibu maswali toka kwa karani wa sensa ya watu na makazi Bw. Clement Ngalaba leo Agosti 26, 2012wakati alipojiunga na mamilioni ya Watanzania katika zoezi hilo lililofanyika kwa mafanikio makubwa nchi nzima.


Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akijiandikisha na familia yake kwa Karani Asia Hassan Mussa,(kushoto) katika zoezi la Sensa ya Watu na  Makazi  lililoanza leo nchini kote.

Rais akiwa katika Shehia ya  Migombani Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja,(kulia ) Mke wa Rais Mama Mwanamwema Shein, [Picha na Ramadhan Othman,Ikulu.]



Makamu  wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, leo Agosti 26, saa tatu asubuhi, ameshiriki kikamilifu zoezi la Sensa ya watu na Makazi akiwa kwenye Makazi yake Oysterbay jijini Dar es Salaam.


Dkt. Bilal, ameshiriki katika zoezi hilo kwa kujibu maswali aliyokuwa akiulizwa na Karani wa Kituo cha Oysterbay, Happyness Masaka, mbaye alifika nyumbani kwa makamu akiwa ameongozana na msimamizi wake, Daria Kailembo, pamoja na Maofisa kutoka Ofisi ya Takwimu ya Taifa, Stanley Mahembe na Radegunda Maro.


Aidha, Dkt. Bilal, ametumia dakika 25 kwa kujibu jumla ya maswali 37, yaliyoandaliwa ili kukamilisha zoezi hilo.


Akizungumza baada ya kukamilisha zoezi hilo, Dkt. Bilal, amewahasa Watanzania wote kwa ujumla kujitokeza na kutoa ushirikiano kwa Makarani ili kufanikisha zoezi hilo, ambalo litadumu kwa siku saba.

Imetolewa na
Ofisi ya Makamu wa Rais
Box 5380
Dar es Salaam.


Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akihojiwa na Karani wa sensa Beatrice Nchimbi  wakati alipojiandikisha kijini kwake Kibaoni, mkoani Katavi, Agust 26,2012.(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu).

Aidha Waziri mkuu Mizengo Pinda amesema posho kwa ajili ya wenyeviti wa vitongoji na vijiji ambao wataambatana na makarani wa sensa zipo palepale na kwamba hawana haja ya kuhofu juu ya malipo yao.

Waziri Mkuu ambaye ni Mwenyekiti wa Kamati ya Kitaifa ya Sensa amewasihi wenyeviti hao waendelee na kazi yao bila wasiwasi wowote kwani watalipwa. 

“Ni kweli malipo yao yamechelewa, ni suala la wikiendi tu kuingilia hapa kati, lakini napenda niwahakikishie kwamba stahili zao zipo, wao wachape kazi tu!” alisisitiza.

Alisema ameona kwenye taarifa za habari kupitia baadhi ya luninga wakidai kwamba wameachwa katika malipo ya kazi hiyo lakini akatumia fursa hiyo kuwahakikishia kwamba watalipwa. “Nimeona kwenye TV wanadai kuwa wameachwa, si kweli. Nawahakikishia wote kwamba wako katika hesabu yetu na wote watalipwa,” aliongeza.



Pia  Waziri Mkuu Pinda aliwaomba Watanzania watambue kuwa zoezi hili lilianza tangu mwaka 2004 na lina gharama kubwa kwani mpaka sasa limegharimu zaidi ya sh. bilioni 140/-.



Alisema ukweli huo unabainishwa na maswali yaliyomo kwenye dodoso la sensa ambayo yanalenga kujua jinsi za watu, umri wao, shughuli zao za kiuchumi na kuwaweka katika makundi ili iwe rahisi kuwahudumia.



Aliwasihi Watanzania ambao hawatahesabiwa leo kuwa wavumilivu kwani zoezi hilo litaendelea kwa muda wa siku saba. “Makarani wataendelea kutembelea kaya kwa siku saba zijazo, cha msingi mkuu wa kaya aandae taarifa za watu waliolala kwenye mji wake usiku wa tarehe 25 kuamkia tarehe 26 Agosti, mwaka huu. Aorodheshe majina yao, umri wao, elimu yao, jinsi zao na shughuli ambazo wanazifanya,” alifafanua.



Kuhusu watu wanaopinga sensa, Waziri Mkuu alisema anaunga mkono kauli zilizotolewa na Rais Jakaya Kikwete pamoja na Rais wa Zanzibar, Dk. Ali Mohammed Shein la kuwataka Watanzania wote washiriki zoezi la sensa.



Aidha kwa upande wake  Mkuu wa mkoa kagera  kanal Mstaafu Fabian Masawe amesema kuwa zoezi la sense ya watu na makazi mkoani Kagera limeanza vizuri  licha ya kwepo kwa  Changamoto ndogondogo   ambazo zinaendelea kutafutiwa ufumbuzi wa haraka.



Akizungumuza Radio Kwizera mkuu huyo wa mkoa  amesema kuwa taalifa kutoka katika wilaya zote 8 za mkoa huo ni kwamba zoezi limenza na hakuna karani aliyekosa vifaa vya kufanyia kazi licha ya kutokuwepo kwa makoti ya kuwatambulisha ambapo vifaa hivyo vinatazamiwa kufika wakati wowote.



Amesema kuwa tatizo la vitambulisho na mabegi ndivyo vilikuwa vikiendelea kugawiwa kutokana na kuchelewa kufika lakini pia suara la fedha limetafutiwa ufumbuzi ambapo zimeanza kusambazwa katika halmashauri zote za mkoa huo.



Hata hivyo amelitaka jeshi la polisi katika wilaya zote mkoani  Kagera  kuhakikisha wanapokea taarifa zote na kuzifanyia kazi haraka ambazo zinaweza kuhatarisha kutofanikiwa kwa zoezi la sense ya watu na makazi ambapo amedai kuwa kuna watu ambao walikuwa wamejipanga kukwamisha zoezi hilo  .



Binafsi nikiwa mmiliki wa Blogger hii,Nawatakieni watanzania  wenzangu Ushiriki mwema wa zoezi la SENSA ya watu na makazi kwa ajili ya kupata takwimu sahihi kwa maendeleo ya Taifa letu.

NAKUSIHI MTANZANIA KUJIOKEZA KUSHIRIKI ZOEZI HILI.




No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad