Meneja
wa Real Madrid Jose Mourinho amesema kuwa Mchezaji wake Cristiano Ronaldo ndie
anastahili kushinda Ballon d'Or na si Mchezaji wa FC Barcelona Lionel Messi.
Aidha
Tuzo ya FIFA Ballon d'Or, au ‘Mpira wa Dhahabu’ huzawadiwa kwa Mchezaji Bora
Duniani kwa Msimu uliopita na Tuzo hii ilianzishwa Mwaka 2010 na huendeshwa na
FIFA pamoja na Gazeti la Ufaransa la Soka liitwalo ‘France Football’ kufuatia
kuunganishwa Tuzo ya FIFA ya Mchezaji Bora Duniani, iliyokuwa ikiendeshwa na
FIFA na Ballon d’Or, iliyokuwa ya France Football.
Mshindi
wa Tuzo hiyo huchaguliwa na Jopo mchanganyiko la Waandishi wa Habari wa
Kimataifa na Makocha wa Timu za Taifa na Makepteni wao.
Mchezaji
Lionel Messi wa FC Barcelona ndie alietwaa Tuzo hii ilipoanzishwa kwa mara ya
kwanza hapo Mwaka 2010 na pia alitwaa Tuzo ya Mchezaji Bora Duniani Mwaka 2009.
Cristiano
Ronaldo, ambae sasa ni Mchezaji wa Real Madrid, alishinda Tuzo hiyo Mwaka 2008
wakati akiwa na Manchester United.
Kocha
Mourinho alisema: “Kwangu mimi, Mchezaji Bora wa Msimu ndie anaeshinda Taji
hilo.” Aliongeza: “Ronaldo ameisaidia Timu kushinda kitu kikubwa na sidhani
katika historia ya Ballon d'Or Mchezaji anatwaa Tuzo bila kushinda kitu
kikubwa. Sasa sidhani Messi bila kushinda CHAMPIONZ LIGI, bila kushinda La
Liga, atatwaa Ballon d'Or.”
Msimu
uliopita, Ronaldo alifunga bao 46 kwenye La Liga na kuiwezesha Real Madrid
kutwaa Ubingwa baada ya kuukosa kwa Miaka minne lakini Messi alikuwa ndie
Mfungaji Bora akiwa na bao 50 huku Barcelona yake ikimaliza nafasi ya pili na
Mwezi Januari Mwaka huu alitwaa Taji la Ballon d'Or kwa mara ya 3 mfululizo.
Mshindi
wa Mwaka 2012 atatangazwa Januari Mwakani.
WASHINDI
WA ZAMANI WA BALLON D'OR:
1956
Stanley Matthews
1957
Alfredo Di Stefano
1958
Raymond Kopa
1959
Alfredo Di Stefano
1960
Luis Suarez
1961
Omar Sivori
1962
Josef Masopust
1963
Lev Yashin
1964
Denis Law
1965
Eusebio
1966
Bobby Charlton
1967
Florian Albert
1968
George Best
1969
Gianni Rivera
1970
Gerd Mueller
1971
Johan Cruyff
1972
Franz Beckenbauer
1973
Johan Cruyff
1974
Johan Cruyff
1975
Oleg Blokhin
1976
Franz Beckenbauer
1977
Allan Simonsen
1978
Kevin Keegan
1979
Kevin Keegan
1980
Karl-Heinz Rummenigge
1981
Karl-Heinz Rummenigge
1982
Paolo Rossi
1983
Michel Platini
1984
Michel Platini
1985
Michel Platini
1986
Igor Belanov
1987
Ruud Gullit
1988
Marco van Basten
1989
Marco van Basten
1990
Lothar Matthaeus
1991
Jean-Pierre Papin
1992
Marco van Basten
1993
Roberto Baggio
1994
Hristo Stoichkov
1995
George Weah
1996
Matthias Sammer
1997
Ronaldo
1998
Zinedine Zidane
1999
Rivaldo
2000
Luis Figo
2001
Michael Owen
2002
Ronaldo
2003
Pavel Nedved
2004
Andriy Shevchenko
2005
Ronaldinho
2006
Fabio Cannavaro
2007
Kaka
2008
Cristiano Ronaldo
2009
Lionel Messi
2010
Lionel Messi
2011
Lionel Messi
No comments:
Post a Comment