Kampuni ya
simu za mkononi ya Vodacom Tanzania imeanzisha ofya mpya ya mwezi mtukufu wa
Ramadhan ambayo itawawezesha wateja wa mtandao huo kupiga simu bila kikomo,
kutuma ujumbe mfupi wa maneno na kupata huduma za intanet kwa shilingi 250/= tu
kwa siku.
Ofa hiyo
mpya itakuwa ni kwa siku saba za wiki kuanzia saa tano usiku hadi saa moja
asubuhi katika kipindi chote cha mwezi mtukufu wa Ramadhan.
Ili mteja ajiunge na huduma hiyo, atatakiwa
kupiga *102*250# ambapo ataweza kupiga simu kutoka Vodacom kwenda Vodacom,
kutuma ujumbe mfupi wa maneno kwenda mitandao yote ya simu na kutumia intanet
bila kikomo.
Akitoa
taarifa kwa vyombo vya habari Mkurugenzi Mtendaji wa Vodacom Tanzania Bwana
Rene Meza alisema kipindi hiki ni maalum kwa waislamu duniani kote kuwa karibu
na Mungu pamoja na ndugu, jamaa na marafiki.
“Tumeona
vyema tuwapatie njia rahisi ya kuwasiliana na ndugu, jamaa na marafiki kwa
unafuu na ambayo wataifurahia tukijua kwamba waislamu walio wengi ni miongoni
mwa wateja ambao wametuunga mkono kwa miaka mingi sasa. Tunataka nao wajisikie
kuwa sehemu ya familia ya Vodacom katika kipindi hiki cha maombi,” alisema
Meza.
Ofa hii
imekuja wakati Vodacom Foundation inaendelea na kampeni yake ya Care and Share
mkoani Tanga inayolenga kutoa misaada ya kifedha na vifaa mbalimbali kwa watoto
yatima katika kipindi cha Mwezi wa Ramadhan.
Kampeni ya
Care and Share inaadhimisha miaka mitano tangu kuzinduliwa kwake, huku ikitoa
fursa ya kipekee kwa Vodacom Foundation kushughulikia changamoto mbalimbali kwa
watoto yatima na vituo vya kulelea watoto yatima.
Kupitia
kampeni hiyo, mamia ya watoto yatima wameweza kusaidiwa na maisha yao
kuboreshwa, suala ambalo jamii nzima na wateja wa Vodacom wanajivunia.
“Tutaendelea
kuwapatia wateja wetu kile wanachostahili kwani bila ya mchango wao Vodacom
Tanzania isingekuwa hapa ilipo leo. Nawatakia waislamu wote kheri katika mwezi
huu mtukufu wa Ramadhan,” alihitimisha Meza.
No comments:
Post a Comment