![]() |
Kutokana na Ukataji na Uchomaji Moto Misitu kukithiri nchini ,Ni vema wadau na jamii kutafuta njia zitakazosaidia kukomesha vitendo vya uchomaji moto misitu nchini. |
Ni jukumu la kila mmoja wetu kutunza mazingira kwani Uchafuzi wa mazingira unasababisha athari nyingi katika jamii.
Mojawapo ya vyanzo vya uchafuzi huo wa mazingira ni uchomaji moto ovyo.
![]() |
Mkuu wa mkoa Kagera licha ya kusisitiza na kutoa maonyo mbalimbali juu ya uchomaji moto ovyo lakini baadhi ya watu wasio na huruma huamua kuchoma moto kama sehemu hii hapa chini inavyoonekana. |
Afisa mazingira wa wilaya ya Ngara mkoani Kagera Bw Mhina Ally Toba amewatahadharisha wafugaji, wakulima na wawindaji kujiepusha na vitendo vya uchomaji moto ovyo katika shughuli zao .
Bw Toba amesema kuwa imekuwa desturi kwa jamii hizo kuchoma moto misitu na mapori mbalimbali hususani wakati wa kiangazi wakijiandaa na shughuli zao ikiwemo kuandaa mashamba, uwinddaji pamoja na kuandaa malisho mapya.
![]() |
Itapendeza sana tukiyatunza mazingira yetu ili yatutunze kama inavyoonekana hapa chini |









No comments:
Post a Comment