Kocha Mkuu wa Yanga Mbelgiji, Tom Saintfiet ametangaza kikosi cha wachezaji 20 watakaocheza michuano ya Kombe la Kagame 2012/2013 - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Friday, July 13, 2012

Kocha Mkuu wa Yanga Mbelgiji, Tom Saintfiet ametangaza kikosi cha wachezaji 20 watakaocheza michuano ya Kombe la Kagame 2012/2013

Kocha wa Yanga, Tom Saintfiet  katikati akizungumza na Waandishi wa Habari, makao makuu ya klabu, Jangwani , kutaja kikosi cha Kombe la Kagame. Kulia ni Katibu Mkuu wa Yanga, Selestine Mwesigwa na kushoto Mwakilishi wa Bia ya Kilimanjaro , wadhamini wakuu wa klabu hiyo, Oscar Shelukindo.
Kocha mkuu wa Yanga, Mbelgiji Tom Saintfiet amewaacha kwenye kikosi kitakachoshiriki michuano ya Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati, Kombe la Kagame kuanzia Jumamosi wachezaji watatu nyota na chipukizi, Omega Seme, Simon Msuva na Frank Damayo kutokana na wachezaji hao kuwa na majukumu ya kitaifa kwa muda mrefu.

Akizungumza na Waandishi wa Habari, makao makuu ya klabu makutano ya Mitaa ya Twiga na Jangwani, Dar es Salaam, Saintfiet alisema kwamba wachezaji hao watakuwa na timu ya taifa ya vijana chini ya umri wa miaka 20, inayojiandaa mechi ya kuwania tiketi ya kucheza Fainali za Mataifa ya Afrika Julai 29 dhidi ya Nigeria.

 

Kocha Tom anasoma majina ya Kikosi cha Yanga

“Kwa  mujibu wa kanuni natakiwa kuwaachia wachezaji siku tano kabla ya mechi, na Jumamosi wanacheza na Rwanda, Jumatatu wanarudiana na Rwanda, baada ya hapo watakuwa kwenye maandalizi ya mechi na Nigeria, kwa hivyo sitakuwa nao hata kwenye Nusu Fainali, kwa sababu hiyo nimeamua kuwaacha,”alisema.

Kocha Saintfiet alisema amemtema pia Nahodha wa klabu hiyo, Nsajigwa Shadrack katika kikosi cha wachezaji 20, lakini amesema mchezaji huyo ni muhimu na atakuwa naye kwenye Ligi Kuu.

 

Mchezaji  Hamis Kiiza

Amewataja wachezaji aliowateua baada ya kushauriana na wasaidizi wake, Freddy Felix Minziro na Mfaume Athumani kuwa ni; makipa Yaw Berko na Ally Mustafa ‘Barthez’, mabeki Juma Abdul, David Luhende, Kelvin Yondan, Nadir Haroub ‘Cannavaro’, Godfrey Taita, Ladislaus Mbogo, Oscar Joshua, Stefano Mwasyika, viungo Athumani Iddi ‘Chuji’, Rashid Gumbo, Juma Seif ‘Kijiko’, Haruna Niyonzima, Shamte Ally, Nizar Khalfan, Idrisa Assenga, Hamisi Kiiza na washambuliaji Said Bahanuzi na Jerry Tegete.

Yanga, ambao ndio mabingwa watetezi wa Kagame, watafungua dimba na mabingwa wa Burundi, Atletico FC Jumamosi Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

 

Makao makuu ya klabu ya Yanga , Jangwani Dar es salaam.
KIKOSI CHA YANGA KAGAME.


Makipa: Yaw Berko na Ally Mustafa ‘Barthez. 

Mabeki: Juma Abdul, David Luhende, Kelvin Yondan, Nadir Haroub ‘Cannavaro’, Godfrey Taita, Ladislaus Mbogo, Oscar Joshua na Stefano Mwasyika. 

Viungo: Athumani Iddi ‘Chuji’, Rashid Gumbo, Juma Seif ‘Kijiko’, Haruna Niyonzima, Shamte Ally, Nizar Khalfan na Idrisa Assenga. 

Washambuliaji: Said Bahanuzi, Hamisi Kiiza na Jerry Tegete.

 

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad