![]() |
Katibu Mtendaji wa Balaza la Mitihani la Tanzania
(NECTA), Dkt. Charles E. Msonde.
Katibu
Mtendaji wa Balaza la Mitihani la Tanzania
(NECTA), Dkt. Charles E. Msonde leo May 6,2018 ameongea na wanahabari
jijini Dar es Salaam na kusema mitiani ya kidato cha sita (ACSEE) na Ualimu Utakaoanza
kesho Jumatatu tarehe 7 hadi 25 Mei,2018.
Jumla ya
Shule za Sekondari 674, Vituo vya Watahiniwa wa Kujitegemea 231 na Vyuo vya Ualimu
125 Tanzania Bara na Zanzibar ambapo Baraza la Mitihani Tanzania (Necta)
limesema Watahiniwa 87,643 wanatarajiwa kufanya mtihani huo wa kidato cha sita.
Akizungumza
na waandishi wa habari amesema kati yao watahiniwa hao, wa shule ni 77,222 na
wa kujitegemea ni 10,421.
Dk Msonde
amesema mtihani utafanyika sambamba na wa kozi ya Ualimu ambao Watahiniwa 7,422
wa Ngazi ya cheti na stashahada wamesajiliwa kuufanya.
"Maandalizi
kwa ajili ya mitihani ya kidato cha sita na ualimu yamekamilika, ikiwamo
kusambaza vijitabu vya kujibia na nyaraka zote muhimu zinazohusu mitihani
hii," amesema Dk Msonde.
![]() ![]() ![]() ![]() ![]() |
Sunday, May 06, 2018

Home
HABARI
Watahiniwa wa shule ni 77,222 na wa Kujitegemea 10,421 kuanza Mitiani kesho Jumatatu Mei 7,2018.
Watahiniwa wa shule ni 77,222 na wa Kujitegemea 10,421 kuanza Mitiani kesho Jumatatu Mei 7,2018.
Tags
# HABARI
Sambaza Hii
Chief Editor | Mhariri
HABARI
Labels:
HABARI
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Kuhusu Mwandishi
Journalist / Chief Editor / Tanzanian Blogger
Simu: 0756830214 / 0620197747 / 0789925630.
No comments:
Post a Comment