Kamanda
Advera Bulimba.
SABABU ZA
KUBAKA
Zipo sababu
kadhaa za watu kujihusisha na ubakaji na ulawiti. Dk Leopord Mwinuka anasema
moja ya sababu hizo ni ‘Pedophilia,’ huo ni ugonjwa wa akili ambao mwanaume
mtu mzima, muda wote anatawaliwa na tamaa ya kufanya mapenzi na mtoto mwenye
umri wa wastani wa miaka kuanzia 12 na zaidi, hata kama ana mbadala wa kufanya
mapenzi na mtu mzima mwingine.
Kwa bahati
mbaya, nchini kuna tatizo la uelewa mdogo kuhusu ‘Pedophilia.’ Watu kwenye
jamii au kazini wanalalamika kuhusu tabia ya mtu ambaye hata wanawake watu
wazima wamtake kimapenzi, hayuko tayari na hisia zake zimejikita kwa watoto.
Wanaougua
maradhi hayo wamekuwa wakitumia pesa, zawadi au lugha za mvuto kuwarubuni
watoto na inaposhindikana, wanaamua kutumia nguvu kufanikisha azma yao.
Sababu
nyingine ni msukumo na tabia ya kuiga kimakundi. Kumekuwapo na tabia ya baadhi
ya vikundi na hasa vijana wanaodhani kwamba kufanya mapenzi na watoto ni sifa.
Hiyo ni tabia mbaya na potofu na baadhi yao wamekuwa wakitumia vilevi kuwapa
hisia katika kufanya tendo hilo.
Baadhi yao,
wamekuwa wakitumia nguvu na vitisho kufanikisha azma yao. Sababu nyingine ni
baadhi ya watu wanaodhani na kuamini kuwa ni rahisi sana kumrubuni kimapenzi
mtoto mdogo kuliko mtu mzima.
Hivyo, kwa
kuwa ameshawahi kujaribu kumtaka kimapenzi mtu mzima akashindwa, anaamua
kufuata watoto akihisi ni rahisi. Mtu huyo anapofanikiwa, mara moja anaendeleza
tabia kwa wengine.
Pia ipo
sababu inayojikita katika dhana ya kulipiza kisasi. Kuna baadhi ya watu
wanaoamua kubaka kwa kuwa alishawahi kulawitiwa alipokuwa mtoto.
Pia zipo
imani za kishirikina kwa waumini wa ushirikina, waliojenga imani kwamba,
kupata utajiri kunafanikishwa kwa njia ya kufanya mapenzi na watoto ambao
wengine wamewazaa.
Tofauti ya
kundi hilo la waumini wa ushirikina na mengine yaliyotangulia, ni kwamba mvuto
mkubwa hujikita kwenye kusaka utajiri.
Katika
makundi yale mengine mali na ushirikina, kinachowavutia ni kufanya mapenzi na
watoto na wanatumia pesa au mali kufanikisha tendo la ngono.
Dalili za
mtoto aliyebakwa, Kulawitiwa
Kuna dalili
nyingi za kumtambua mtoto aliyebakwa au kulawitiwa moja ikiwa mtoto kuwa na
woga uliopitiliza kwa mtu au ndugu ambaye zamani hakuwa akimuogopa na
anapoulizwa, anakuwa mzito kutoa sababu.
Anakuwa
katika namna kwamba ametishwa asiseme, au kuna onyo la siri kwamba akisema
ataadhibiwa na wazazi au walezi anatambua kwamba ni kitendo kibaya.
Kuna baadhi
wanaogopa sana kubadili nguo mbele za watu, wakati zamani kabla ya tukio hilo,
walifanya hivyo kwa uhuru mkubwa.
Kuna watoto
ambao wakishabakwa au kulawitiwa, hubadili hata namna ya kulala na wanakosa
usingizi wakitawaliwa na mawazo na kutafakari kilichowatokea na hatari ya
kukabiliwa tena na balaa hilo.
Watoto hao
wanafikia hatua ya kuota ndoto mbaya na za kutisha. Anaota mtu anamfanyia tendo
lililomtokea, ikiwa ni pamoja na kutawaliwa na hisia za historia ambayo
kitaalamu inaitwa ‘flashback.’
Pia, watoto
waliobakwa au kulawitiwa wanakuwa na tabia ya kulala mchana, wakati wa masomo
shuleni, yeye anabaki akisinzia au kulala, tabu ambayo hakuwa nayo huko nyuma.
Katika
maendeleo ya kitaaluma, mtoto anaanguka ghafla, wakati huko nyuma alikuwa na
maendeleo mazuri darasani.
Hiyo hutokea
hata kuwa mtihani kwa walimu, wazazi na walezi kupata tabu kutambua sababu za
haraka zinazofanya kutokea mabadiliko hayo.
Pia ni
kawaida ya wanafunzi wenzake shuleni wanalalamika na mabadiliko yake ya tabia,
kwani aliyebakwa anapoteza kabisa hamu ya vitu au michezo ambayo alikuwa
akiipenda sana huko nyuma.
Kuna baadhi
ya watoto waliobakwa, hubadili namna ya kutembea au kukaa na hasa kutokana na
maumivu katika sehemu zao za siri, kulingana na mahali alikojeruhiwa.
|
Tuesday, March 20, 2018
Tatizo la Ubakaji,Ulawiti kwa Watoto ni Janga.
Tags
# HABARI
Sambaza Hii
Chief Editor | Mhariri
HABARI
Labels:
HABARI
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Kuhusu Mwandishi
Journalist / Chief Editor / Tanzanian Blogger
Simu: 0756830214 / 0620197747 / 0789925630.
No comments:
Post a Comment