Vita Dawa za Kulevya Tanzania: Rc Makonda na Majina ya wala unga na wafanyabiashara, wako wasanii na askari 9 - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Thursday, February 02, 2017

Vita Dawa za Kulevya Tanzania: Rc Makonda na Majina ya wala unga na wafanyabiashara, wako wasanii na askari 9


Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam,Bw. Paul Makonda amewataja Askari 9 wanaotuhumiwa kushirikiana na Wafanya biashara ya Madawa ya kulevya.

Aidha amewataja wasanii wanaojihusisha na matumizi na uuzaji wa Madawa ya kulevya na kuwataka kuripoti kituo cha Polisi  hapo kesho February 03,2017.

Akiongea na waandishi wa habari akiwa ofisini kwake Alhamisi hii,February 02,2017, RC Makonda amewataka wauzaji wote kufika makao makuu ya Polisi kwajili ya kujieleza.

“Nimeamua kuingia kwenye hii vita kwa sababu najua siku moja Mungu ataniuliza, nilikupa mkoa wa Dar es salaam kupitia Rais John Pombe Magufuli watoto waliangamia kwa Madawa ya kulevya, sitaki kufika mbungini nisiwe na jibu, nipo tayari kupoteza ukuu wangu wa mkoa, nipo tayari kutangulia kwa aliyeniumba lakini niwe na jibu kwa mungu wangu aliyeniumba kwamba Madawa ya kulevya hayakubaliki ndani ya Dar es salaam,” alisema Makonda.

Aliongeza,’Wapo tuliowakamata pamoja na dawa zao tumeshawafikisha Central Polisi na wanaendelea na mambo yanayotakiwa

Lakini wapo ambao bado, majina ni mengi sana mtayapitia wenyewe, kuna Mchafu, Director Joan, Mirror, Rommy na wengine wengi, wapo wauzaji wadogo na wengine wakubwa. 

Lakini wapo wengine wanasemekana wanatumia lakini hakuna ushahidi kwamba wanatumia ingiwa wenzao wanasema wanatumia, ni bora nikakutana nao kesho pale Central, akiwemo TID, Wema Sepetu,”

List ya Watuhumiwa iko hapa Chini.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad