Waziri wa
mashauri ya nchi za kigeni wa Chad Moussa Faki.
Waziri wa
mashauri ya nchi za kigeni wa Chad Moussa Faki amechaguliwa kuwa mwenyekiti
mpya wa tume ya Muungano wa Afrika AU.
Faki
anachukua mahala pake Dlamini Zuma kutoka Afrika Kusini ambaye kipindi chake
cha kuhudumu kimekamilika.
Mshindani
,mkuu wa Bwana Faki katika duru ya mwisho ya upigaji kura, wakati wa kikao cha
AU mjiji Addis Ababa, Ethiopia, alikuwa ni waziri wa mashauri ya nchi za kigeni
wa Kenya Amina Mohamed.
Wagombea
watano waliokuwa wakiwania wadhifa huo ni pamoja na waziri wa mambo ya nchi za
kigeni wa Kenya Amina Mohammed, mwanadiplomasia Abdoulaye Bathily kutoka
Senegal, waziri wa mashauri ya nchi za kigeni wa Chad Moussa Faki Mahamat,
mwanasiasa mkongwe kutoka Botswanda Pelonomi Venson-Moitoi na aliyekuwa wakati
mmoja mshauri wa rais wa Equatorial Guinea Mba Mokuy.
|
No comments:
Post a Comment