Makatibu wa UVCCM Ngazi za Wilaya Nchini watakiwa kuanzisha Jogging Club ili kusimamia kauli mbiu ya 'MAZOEZI KWA AFYA' - Mwana Wa Makonda
cV7ufzj

Muhtasari

X-BET

MAIN-

Post Top Ad

cV7ufzj

Saturday, December 24, 2016

demo-image

Makatibu wa UVCCM Ngazi za Wilaya Nchini watakiwa kuanzisha Jogging Club ili kusimamia kauli mbiu ya 'MAZOEZI KWA AFYA'

.com/simgad/
4
Kaimu katibu Mkuu UVCCM Taifa, Shaka Hamdu Shaka wa pili kulia akiendelea na Zoezi la Unyooshaji wa Viungo pamoja na Mkuu wa Mkuu wa Wilaya ya Karagwe,Mkoani Kagera Mhe. Godfrey Ayub  Mheluka.

7
 Kaimu katibu Idara ya Hamasa,Sera,Utafiti na Mawasiliano Ndg Mtemi Slyvester Yaredi akiendelea na zoezi la kunyoosha viungo.

6
Kijasho chembamba kikimtiririka Mwenyekiti wa UVCCM Mkoa wa Kagera Ndg:Yahya Kamteme katika zoezi la unyooshaji wa Viungo Vya Mwili katika Viwanja Vya CCM Wilaya ya Karagwe,mkoani Kagera.

1
Kaimu katibu mkuu Uvccm Taifa ndg Shaka H.Shaka leo amezindua rasmi kampeni ya Jogging UVCCM yenye kauli mbiu ya 'MAZOEZI KWA AFYA' iliyozinduliwa Kitaifa Wilayani Karagwe mkoani Kagera.

Katika Mazozi hayo Kaimu katibu mkuu ameshiriki Jogging na Mazoezi Viungo akiongozwa na Mwenyekiti  Uvccm mkoa wa Kagera ndg YAHYA KATEME,Mkuu wa Wilaya Karagwe  Mhe. Godfrey Ayub  Mheluka pamoja na vijana na viongozi mbalimbali  Wa Chama na Serikali Wilayani humo. 

Akiongea  mara baada ya Mazoezi hayo Ndg: Kaimu katibu mkuu UVCCM Taifa ,Shaka Hamdu Shaka amewataka Makatibu wa UVCCM Ngazi za Wilaya Nchini kote kuzingatia maelekezo yaliyotolewa tangu Mnamo tarehe 24 Mwezi Oktoba 2016 ya kuanzisha jogging Club alisema "nitumie fursa hii kuwapongeza sana kwa kutambua umuhimu wa mazoezi, sasa Vijana lazima wawe wakakamavu na tayari muda wote hatuwezi kuwa na taifa la vijana goigoi wasio jiweza kama ambavyo  hata makamu wa Rais alivyounga mkono katika swala hili la mazoezi.

 " Pia amewataka vijana wote kushiriki ipasavyo Zoezi hili amesema '' Jogging ni swala muhimu sana kwa vijana kwani pamoja na kujenga miili yetu jogging itatufanya tuwe wamoja t wenye ushirikiano wa kudumu haswa katika mambo mbali mbali ya kijamii''.

 Kaimu katibu mkuu yupo katika ziara ya siku nane mkoani Kagera ambapo atatembelea wilaya zote 8 za mkoa wa Kagera.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad

Contact Form

Name

Email *

Message *