LEWIS GABRIEL Toka Kata ya Chanika wilayani Karagwe/Kagera Ndiye Mshindi wa RADIO KARAGWE STAR SEARCH 2016. - Mwana Wa Makonda
cV7ufzj

Muhtasari

X-BET

MAIN-

Post Top Ad

cV7ufzj

Saturday, December 17, 2016

demo-image

LEWIS GABRIEL Toka Kata ya Chanika wilayani Karagwe/Kagera Ndiye Mshindi wa RADIO KARAGWE STAR SEARCH 2016.

.com/simgad/
IMG_20161217_012209

Pichani ni Mashabiki wa Msanii LEWIS GABRIEL Kutoka Kata ya Chanika wilayani Karagwe wakifurahia ushindi wa Msanii wao huyo aliyeibuka kidume katika Shindano la Kituo cha Radio Karagwe kilichopo wilayani Karagwe mkoani Kagera kupitia Shindano la RADIO KARAGWE STAR SEARCH 2016 ambapo aliwashinda washiriki wenzake kwa kupata asilimia 96 YA Kura za Majaji.

Fainali ya mashindano hayo imefanyika jana Ijumaa December 16,2016 na Vigezo vilivytazamwa na Majaji kwa Washiriki wote 31 kutoka wilaya nne za mkoa wa Kagera za Karagwe, Misenyi, kyerwa na Bukoba vijijini  ni pamoja na Muonekano, Ubunifu, maudhui ya wimbo/ujumbe, melod/ghani, hamasa, Uchangamfu na kutawala jukwaa, Uwezo wa kutoa sauti halisi.
IMG_20161217_012214
Aidha kuelekea Fainali hiyo,Jumla ya washiriki nane waliingia katika  hatua hiyo na Matokeo kutolewa kama ifatavyo.

MSHINDI WA KWANZA: Lewis Gabriel 96% -Kata ya Chanika wilaya ya Karagwe. 

MSHINDI WA PILI: Efatha Band 76% -Kutoka  wilaya Kyerwa. 


MSHINDI WA TATU:Merchades Kazoba 70% -Kutoka wilaya ya Kyerwa.
IMG_20161217_085721

Mgeni rasmi Mhe. Karim Amri ambaye ni MNEC Wilaya ya Karagwe (Pichani kushoto ) Katika fainali hiyo ya  RADIO KARAGWE STAR SEARCH 2016  pamoja na kutoa Zawadi ya cheti kwa washiriki wote.

Licha ya kuwapongeza Washiriki wote kwa kushiriki vyema na kuoneshana ushindani kupitia vipaji vyao aliwataka Washiriki wa shindano hilo kutunga wimbo kuhusu Utunzaji  wa mazingira na uhifadhi wake, na kuahidi kuudhamini wimbo huo na video yake ili kuhamasisha Wana Karagwe kuhifadhi na kutunza mazingira
IMG_20161217_003132
Mgeni rasmi Mhe. Karim Amri ambaye ni MNEC Wilaya ya Karagwe (Pichani kulia)sambamba na Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Karagwe na Diwani wa kata ya Rugera Mhe.Dawson Byamanyilohi wakifatilia kwa umakini shindano hilo.

IMG_20161217_003317

IMG_20161217_005539
Meza ya Majaji wakati wa shindano la Radio Karagwe Star Search 2016 lililohitimishwa jana December 16,2016 Mjini Kayanga,Karagwe.
IMG_20161217_005729

IMG_20161217_005801
Washiriki kama kawaida walipandishwa Kikaangoni kujajiwa.

IMG_20161217_011140

IMG_20161217_011142
Mashabiki hawakuwa nyuma nao kufatilia kila kitu wakati wa fainali hiyo.

IMG_20161217_011146

IMG_20161217_012106

IMG_20161217_012912

IMG_20161217_012955

IMG_20161217_013146
Pichani juu na chini ni Mgeni rasmi Mhe. Karim Amri ( (Pichani kulia) ambaye ni MNEC Wilaya ya Karagwe akigawa zawadi ya Vyeti kwa Washiriki nane wa fainali katika shindano hilo.

IMG_20161217_013227

IMG_20161217_013325

IMG_20161217_013326

IMG_20161217_014304

Kutoka katikati ni Mkurugenzi wa Radio Karagwe, Dkt. Godfrey Aligawesa,pamoja na kuwashukuru wadau kwa kuchangia udhamini wao na kuhudhuria,amesema  lengo lilikuwa ni kumpata msanii chipukizi atakayesimamiwa na Kituo hicho cha redio  kurekodi  wimbo wake atakaokuwa ameutunga na album yake.

kushoto ni Bw. Shaban Ngallama Afisa uzalishaji Vipindi Radio Karagwe.
IMG_20161217_001233

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad

Contact Form

Name

Email *

Message *