Ligi kuu Vodacom 2016/2017 - Yanga SC yaondoka na mabao 3-0 dhidi ya Majimaji. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Saturday, September 10, 2016

Ligi kuu Vodacom 2016/2017 - Yanga SC yaondoka na mabao 3-0 dhidi ya Majimaji.

Mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara kati ya Yanga SC dhidi ya Majimaji unachezwa leo ,Septemba 10,2016 kwenye Uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam na Yanga  SC inaondoka na ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Majimaji.

 Mfungaji bora wa Ligi Kuu msimu uliopita, Amissi Joselyn Tambwe alifunga mabao mawili kipindi cha pili baada ya kiungo Deus David Kaseke kutangulia kufunga kipindi cha kwanza.
Yanga sasa inafikisha pointi saba, baada ya kucheza mecni tatu, ikishinda mbili na sare moja – sawa na mahasimu wao, Simba SC.

Mechi nyingine za Ligi Kuu leo,Jumamosi- Mwadui FC imelazimishwa sare ya 2-2 na ndugu zao Stand United Uwanja wa Mwadui Complex, Shinyanga, Mbeya City imefungwa nyumbani 2-1 na Azam FC na Ndanda FC imelazimishwa sare ya 0-0 na Kagera Sugar, Ruvu Shooting imewalza ndugu zao JKT Ruvu 1-0 Uwanja wa Mabatini, Mlandizi Pwani.

LIGI KUU VODACOM -2016/2017.

Jumapili Septemba 11, 2016.

Simba SC v Mtibwa Sugar

Tanzania Prisons v Toto Africans

Jumapili Septemba 12, 2016.

African Lyon v Mbao FC

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad