Wakazi wa
Vijiji Nyagwijima, Mugunzu na Kakonko wilaya
Kakonko Mkoani Kigoma wameiomba serikali kuwaboreshea miundo mbinu ya
maji ili waweze kuondokana na Tatizo la uhaba wa maji kwenye vijiji vyao kwa
kutembea mwendo mrefu wakitafuta bidhaa hiyo hatua inayowakwamisha katika
shughuli zao za uzalishaji mali.
Wakiongea na
Waandishi wa Habari kwa nyakati tofauti
baadhi ya wananchi ambao ni
Rosemary Rafael na Secelie Ntungie wamesema
katika maeneo mengi ya vijijini ambako ndiko nguvu kazi kubwa ya uzalishaji mali iliko,
kuna shida kubwa ya maji nakueleza kuwa magati
mengi ya kutolea maji yamesimikwa
tu bila kutoa maji na kulazimika kuyafuata umbali mrefu.
‘’ Serikali
imekuwa ikielekeza nguvu nyingi kwa huduma mbalimbali ikiwemo maji katika
maeneo ya Mijini tofauti na vijijini hatua inayopelekea shughuli za uzalishaji
mali kutokuwa na mafanikio mazuri kwa kuwa wananchi wengi hasa majira ya
kiangazi maeneo mengi ukauka na kuwalazimu kutumia muda mwingi wakitafuta maji
alisemaalisema Rosemary’’
Pamoja na
wananchi kuhangaika kutafuta maji, upo mradi wa maji unaofadhiliwa na Benk ya Dunia katika vijiji
ambapo kama taratibu zingewekwa vizuri, uenda
unafuu ungepatikana kwa wananchi, ambapo Madiwani katika kikao cha
Baraza hilo kwa ajili ya kujadili mswala ya maendeleo ya wananchi wamesema kutokana na wilaya ya kibondo
kutokabidhi miradi ya maji kwa wilaya ya Kakonko kumesababisha usumbu wa kukosa
maji, kwa sababu hapo awali kabla ya
wilaya kugawanywa iliku ikisimamiwa na wailaya ya kibondo hadi sasa.
|
No comments:
Post a Comment