HOTUBA YA RAIS MAGUFULI:-Uwekaji wa Jiwe la Msingi la ujenzi wa FLYOVER Jijini Dar es Salaam April 16,2016. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Sunday, April 17, 2016

HOTUBA YA RAIS MAGUFULI:-Uwekaji wa Jiwe la Msingi la ujenzi wa FLYOVER Jijini Dar es Salaam April 16,2016.

Mkurugenzi Mtendaji wa Wakala wa Barabara Nchini (TANROADS), Eng. Patrick Mfugale akitoa maelezo kwa Rais, Dkt. John Pombe Magufuli, wakati wa hafla ya uwekaji wa jiwe la Msingi ujwenzi wa Barabara ya Juu (FlyOver) kwenye makutano ya Barabara ya Mandela na Nyerere, eneo la Tazara, Jijini Dar es salaam.

****


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt John Magufuli ameweka jiwe la msingi kwa ajili ya kuanza  rasmi ujenzi wa barabara ya juu kwenye makutano ya barabara za Nyerere na Mandela eneo la Tazara jijini Dar es Salaam leo.

Akizungumza katika uzinduzi huo, Rais Magufuli amesema ujenzi huo wa barabara ya juu utaanza mara moja kwa ushirikiano na serikali ya Japan  na utagharimu Shilingi 100 bilioni.

Amesema, serikali ya Japan imefadhili mradi huo kwa Sh 93.44 bilioni wakati serikali ya Tanzania imechangia Sh 8.36 bilioni na unatarajiwa kukamilika ifikapo Oktoba 2018.


No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad