![]() |
|
WATU elfu 18 na 887 sawa na
asilimia 4 wamekutwa na maambukizi ya
Virusi vya UKIMWI, kati ya watu Laki 4,
elfu 77 na 493 ambao walijitokeza kupima virusi vya Ukimwi kwa hiari katika mkoa wa Kagera
kwa mwaka 2015 / 2016.
Afisa Maendeleo
ya Jamii mkoani Kagera ,Bw Charles Mafyimbo amesema hayo wakati akiongea na Wanahabari, ofisini kwake juu hali ya maambukizi ya virusi vya Ukimwi
ilivyo kwa sasa katika mkoa wa Kagera.
Amesema katika wilaya
za mkoa wa Kagera, wilaya ya
Bukoba vijijini inaogoza kwa maambukizi
ya virusi vya UKIMWI kwa kuwa na asilimia 6.0 ikifuatia
na wilaya ya Muleba
ambayo ina asilimia 5.5 huku
Manispaa ya Bukoba ikiwa na asilimia
4.6 na kwamba wilaya ya Ngara maambukizi ya virusi vya ukimwi yameshuka kwa asilimia 2.3 tofauti na mwaka 2014
ilikuwa asilimia2.6.
Hata hivyo
Bw Mafyimbo amesema elimu inaendelea kutolewa kwa Jamii huku akitaja wilaya zinazongoza kwa maabukizi ya
ukimwi zina mwingiliano wa watu wakiwemo kutoka Visiwani ,Bandarini ikiwemo Kemondo na
maeneo ya mipakani ya Kabanga,Rusumo wilayani Ngara na Mtukula wilayani Misenyi.
Pata Picha, Habari za Siasa, Kijamii, Biashara, Muziki na Michezo na Nyingine kwa kujiunga na Mimi Hapa...FACEBOOK .. TWITTER .. INSTAGRAM … Pia Usisite kututumia tukio la Picha/Habari kwa WhatsApp +255789925630 Or +255756830214.
|
Tuesday, February 23, 2016
Home
HABARI
MAAMBUKIZI YA UKIMWI KAGERA:-Wilaya ya Bukoba vijijini yaongoza mkoani Kagera kwa asilimia 6.0...Ngara kwa asilimia 2.3.
MAAMBUKIZI YA UKIMWI KAGERA:-Wilaya ya Bukoba vijijini yaongoza mkoani Kagera kwa asilimia 6.0...Ngara kwa asilimia 2.3.
Tags
# HABARI
Sambaza Hii
Chief Editor | Mhariri
HABARI
Labels:
HABARI
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Kuhusu Mwandishi
Journalist / Chief Editor / Tanzanian Blogger
Simu: 0756830214 / 0620197747 / 0789925630.






No comments:
Post a Comment