Uhamiaji Kagera Yazindua Pasipoti za Kielekitroniki leo Juni 8, 2018 na Hivi Ndivyo vinahitajika ili Upate Pasipoti. - Mwana Wa Makonda
cV7ufzj

Muhtasari

X-BET

MAIN-

Post Top Ad

cV7ufzj

Friday, June 08, 2018

demo-image

Uhamiaji Kagera Yazindua Pasipoti za Kielekitroniki leo Juni 8, 2018 na Hivi Ndivyo vinahitajika ili Upate Pasipoti.

.com/simgad/
Kamishna%2Bwa%2BUraia%2Bna%2BPasipoti%2BGerald%2BKihinga%2B%2528Kushoto%2529%2BAkimkabidhi%2BKaimu%2BMkuu%2Bwa%2BMkoa%2Bwa%2BKagera%2BMhe.%2BKinawilo%2B%2BPasipoti%2Bya%2BKielekitroniki%2BBaada%2Bya%2BUzinduzi%2B%2B
Kamishna wa Uraia na Pasipoti Gerald Kihinga (Kushoto) Akimkabidhi Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Kagera Mhe. Kinawilo  Pasipoti ya Kielekitroniki Baada ya Uzinduzi.  

Na: Sylvester Raphael.

Mkoa wa Kagera umezindua rasmi Pasipoti za Kielekitroniki leo Juni 8, 2018 katika viwanja vya Uhuru Manispaa ya Bukoba ambapo Pasipoti hizo zimezinduliwa na kutolewa kwa mara ya kwanza  Mkoani Kagera kwa Viongozi na Wananchi wa kawaida na Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Kagera Mkuu wa wa Wilaya ya Bukoba  Mhe. Deodatus Kinawilo.

Kwaniaba ya Mkuu wa Mkoa wa Kagera Meja Jenerali Mstaafu Salum M. Kijuu , Mhe Deodatus Kinawilo katika uzinduzi huo, alisema kuwa Mkoa wa Kagera unajivunia kuzindua Pasipoti za Kielekitroniki  kwani sasa wananchi wake watapata Pasipoti zinazotambulika Kimataifa na zenye uhakikaka zaidi.

Mhe. Kinawilo alisema kuwa Pasipoti ya Kielekitroniki inayo mambo muhimu makuu manne tofauti na Pasipoti  ya zamani kama ifuatavyo;-

KWANZA - Ni pasipoti inyomtambulisha Mtanzania katika Jumuiya ya Afrika Mashariki na Kimataifa,  kwahiyo Pasipoti ya Afrika Mashariki haitatolewa tena bali itatumika Pasipoti  moja ya Kielekitroniki tu.

PILI - Pasipoti ya Kielekitroniki inazo alama za kiusalama ambazo si rahisi kuzigushi. 

TATU - Pasipoti ya Kielekitroniki ni ya Kimataifa ambayo hahitaji ulazima wa ukaguzi bali mtu mwenye nayo anaweza kupita kwenye mitambo maalum na kujulikana kuwa ni Mtanzania. 

NNE - Pasipoti ya Kielekitroniki inayo program maalum ambayo mwananchi anaweza kuitunza kwenye simu yake na kama Pasipoti yake ikipotea ghafla anaweza kuitumia aliyoitunza kwenye simu yake.

Mwisho Kaimu Mkuu wa Mkoa Mhe. Kinawilo alitoa tahadhari kwa Watumishi wa Idara ya Uhamiaji kuwa makini wakati wa kutoa Pasipoti za Kielekitroniki kwa wananchi ambao ni Watanzania tu na siyo kuzitoa kwa wasio raia wa Tanzania. 

Pia alitoa wito kwa Maafisa wa Idara ya Uhamiaji kuwasaidia wananchi watakaohitaji Pasipoti hizo na hawana uelewa wa kutumia kompyuta ili wasaidiwe kujaza fomu zao.
Kaimu%2BMkuu%2Bwa%2BMkoa%2BMhe%2BKinawli%2BAkimkabidhi%2BPasipoti%2Bya%2BKielekitroniki%2BBaba%2BAskofu%2BLwoma%2Bwa%2BAskofu%2BMkuu%2Bwa%2BJimbo%2Bla%2BBukoba
Kaimu Mkuu wa Mkoa Mhe Kinawli Akimkabidhi Pasipoti ya Kielekitroniki Baba Askofu Lwoma wa Askofu Mkuu wa Jimbo la Bukoba.
Katibu%2BTawala%2BMkoa%2BKagera%2BCP%2BDiwani%2BAthuman%2BAkisubiri%2BKuchukuliwa%2BAlama%2Bza%2BVidole%2BKukamilisha%2BHatua%2Bza%2BPasipoti%2Bya%2BKielekitroniki%2B
Katibu Tawala Mkoa Kagera CP Diwani Athuman Akisubiri Kuchukuliwa Alama za Vidole Kukamilisha Hatua za Pasipoti ya Kielekitroniki.
Mkuu%2Bwa%2BMkoa%2BKagera%2BMhe.%2BKijuu%2Bna%2BKatibu%2BTawala%2BMkoa%2BCP%2BDiwani%2BAthuman%2BWakishiriki%2BHatua%2Bza%2BKupata%2BPasipoti%2Bya%2BKielekitroniki
Mkuu wa Mkoa Kagera Mhe. Kijuu na Katibu Tawala Mkoa CP Diwani Athuman Wakishiriki Hatua za Kupata Pasipoti ya Kielekitroniki.

Awali  Kamishina wa Uraia na Pasipoti Gerald Kihinga alisema kuwa mara baada ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.John Pombe Magufuli kuzindua Pasipoti za Kielekitroniki Januari 31, 2018 Pasipoti hizo zilikuwa zinatolewa Makao Makuu ya Uhamiaji Dar es Salaam na Zanzibar  tu lakini sasa mikoa imeanza kuzindua na kutoa Pasipoti za Kielekitroniki.

Kamishna Kihinga alisema kuwa tayari Pasipoti za Kielekitroniki zimeanza kutolewa katika mikoa ya Dadoma, Dar es Salaam, Arusha, Kilimanjaro na sasa Mkoa wa Kagera ambao uzinduzi umefanyika leo Juni 8, 2018. 

Jumla ya Pasipoti za Kielekitroniki 17,595; zimetolewa  huku Pasipoti za Kielekitroniki za kawaida zikiwa 17,289 za Utumishi 56, za Kidiplomasia 248, na Diplomasia Maalum mbili tu.
Askofu%2BMkuu%2Bwa%2BJimbo%2BKatoriki%2Bla%2BBukoba%2BDesiderius%2BLwoma%2Bna%2BAskofu%2BMsaidizi%2BKilaini%2BWakifurahia%2BPasipoti%2Bzao%2Bza%2BKielekitriniki%2BBaada%2Bya%2BKuzinduliwa%2BRasmina%2BKukubidhiwa
Askofu Mkuu wa Jimbo Katoriki la Bukoba Desiderius Lwoma na Askofu Msaidizi Kilaini Wakifurahia Pasipoti zao za Kielekitriniki Baada ya Kuzinduliwa Rasmina Kukubidhiwa.
Askofu%2BMsaidizi%2Bwa%2BJimbo%2BKatoriki%2Bla%2BBukoba%2BAkitoa%2BNeno%2Bla%2BShukrani%2BBaada%2Bya%2BUzinduzi%2Bna%2BKukabidhiwa%2BRasmi%2BPasipoti%2Bza%2BKielekitroniki%2BMkoani%2BKagera
Askofu Msaidizi wa Jimbo Katoriki la Bukoba Akitoa Neno la Shukrani Baada ya Uzinduzi na Kukabidhiwa Rasmi Pasipoti za Kielekitroniki Mkoani Kagera.


Kwaniaba ya Viongozi na wote waliopatiwa Pasipoti za Kielekitroniki katika uzinduzi Mkoani Kagera Baba Askofu Methodius Kilaini ,Askofu Msaidizi wa Jimbo Katoriki la Bukoba aliishukuru Serikali na Idara ya Uhamiaji kwa kutoa Pasipoti za Kielekitroniki kwa wananchi na alisema kuwa Idara ya Uhamiaji Mkoa wa Kagera imejipanga vizuri hasa katika mapokezi ya wananchi na huduma.


Tunashukuru sana na nimeikagua Pasipoti yangu ya Kielekitroniki na kugundua kuwa ni pasipoti nzuri sana tena  sana, sasa itatusaidia sisi kama Viongozi wa dini na wananchi katika kusafiri, naiona Tanzania ikiendana na mataifa mengine katika masuala ya mitandao.” Alisistiza Baba Askofu Kilaini. 
Kaimu%2BMkuu%2Bwa%2BMkoa%2Bwa%2BKagera%2BMhe.%2BDeodatus%2BKinawilo%2BAkisoma%2BHotuba%2Bya%2BUzinduzi%2Bwa%2BPasipoti%2Bya%2BKielekitriniki%2BMkoani%2BKagera%2BKwaniba%2Bya%2BMkuu%2Bwa%2BMkoa
Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Kagera Mhe. Deodatus Kinawilo Akisoma Hotuba ya Uzinduzi wa Pasipoti ya Kielekitriniki Mkoani Kagera Kwaniba ya Mkuu wa Mkoa.
Maofisa%2Bwa%2BIdara%2Bya%2BUhamiaji%2BWakisikiliza%2BKwa%2BUmakini%2BHotuba%2Bya%2BUzinduzi%2Bwa%2BPasipoti%2Bza%2BKielekitroniki%2BMkoani%2BKagera
Maofisa wa Idara ya Uhamiaji Wakisikiliza Kwa Umakini Hotuba ya Uzinduzi wa Pasipoti za Kielekitroniki Mkoani Kagera.

Naye Afisa Uhamiaji wa Mkoa wa Kagera Abdalah Towo akiongea na mhadhara wa wananchi waliohudhuria uzinduzi wa Pasipoti za Kielekitroniki aliwakumbusha Maafisa wenzake katika Wilaya kuwa Elimu imetolewa ya kutosha kwao na ni lazima kuwaelimisha wananchi na kuwaongoza katika kupata Pasipoti za Kielekitroniki katika Wilaya zao.

 Pia Bw. Towo alitoa rai kwa wananchi waliopatiwa Pasipoti za Kielekitroniki katika uzinduzi huo kuwa mabalozi wazuri wa kuwaelimisha wenzao na kuhakikisha wanapitia michakato yote wao waliyoipitia na kama kutatokea mwananchi anasema yeye hajapitia mchakato huo na amepata Pasipoti ya kielekitroniki aripotiwe mara moja katika Ofisi za Uhamiaji ili hatua zichuliwe mara moja.

Aidha, Bw. Towo alisema katika uzinduzi huo zilitolewa Pasipoti za Kielekitroniki 101 kwa Viongozi wa Serikali, Viongozi wa Dini, Wazee, Watumishi na Wananchi. 

Rai kwa wananchi kwa kuwa Mkoa wa Kagera umepakana na nchi tatu ni lazima wananchi kutoa ushirikiano wa kutoa taarifa ili Pasipoti za Kielekitroniki zisitolewe kwa wasiokuwa raia wa Tanzania.
Picha%2Bya%2BPamoja%2B
Picha ya Pamoja .

Unahitaji nini ili Upate Pasipoti ya Kielekitroniki?

Gharama ya Pasipoti ya Kielekitroniki ni Shilingi 150,000/=, Utajaza fomu hata ukiwa nyumbani ambayo inapatikana katika tovuti ya Idara ya Uhamiaji www.immigration.go.tz

Viamabatanisho ni pamoja na Kitambulisho cha Taifa, Cheti cha kuzaliwa cha kwako na cha mzazi wako mmoja, Barua ya utambulisho kutoka kazini kwako/Mtendaji wa kata, Kitambulisho cha Kazi/mpiga kura, na picha tatu pasipoti size.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad

Contact Form

Name

Email *

Message *