Taharuki Kumuzuza,Ngara baada ya Madai ya Vifo na Nyumba Kuungua Kimiujiza. - Mwana Wa Makonda
cV7ufzj

Muhtasari

X-BET

MAIN-

Post Top Ad

cV7ufzj

Friday, June 08, 2018

demo-image

Taharuki Kumuzuza,Ngara baada ya Madai ya Vifo na Nyumba Kuungua Kimiujiza.

.com/simgad/
34687474_1886232618083306_2041870552515215360_n
Kaimu Mwenyekiti wa Kijiji cha Kumuzuza Bw Marthon Christopher akionesha moto ulivyounguza Nyumba ya Mzee Petro huku baadhi ya Wananchi wakishuhudia.
34664666_1886232674749967_6297282093072252928_n
 Nyumba saba zimeungua kwa nyakati tofauti katika kijiji cha Kumuzuza wilayani Ngara mkoani Kagera huku kukitokea vifo vya watoto wawili ndani ya familia moja katika Mazingira ya kutatanisha vikihusishwa kwa imani za kishirikina. 

 Kaimu Mwenyekiti wa Kijiji cha Kumuzuza Bw Marthon Christopher amesema Mtoto wa kwanza amefariki mwezi mmoja uliopita na mwingine amefariki juzi na wote ni wajukuu wa mzee mmoja aitwaye Petro Sabimihana mwenye umri wa miaka 68.

  Bw Christopher amesema watoto waliofariki mmoja ana umri wa miaka minane mwingine miaka miwili na kukutwa chumbani ndani ya nyumba ya mzee huyo ikiwa imefungwa na kwamba nyumba saba zimeungua kuanzia Novemba mwaka jana (2017) na iliyoungua jana chanzo chake hakijafahamika.
 34673617_1886232628083305_7334660469086486528_n
34775037_1886232604749974_4340191222862708736_n
Kwa upande wake Mzee Petro Sabimihana alikiri kuijiwa na miujiza na kuunguliwa na vitu mbalimbali ndani ya nyumba yake na kwamba hadi sasa hana nguo, chakula wala vyombo na moto huo huunguza majiko, vyoo bila kujua chanzo chake.

 Alisema alijitahidi kufanya maombi akisaidiwa na Padri Pamphilius Kitondo ikashindikana ambapo miujiza hiyo hupoteza wajukuu wake kupitia chumba anacholala hata kama kimefungwa hukuta wamefariki.
 34818934_1886232698083298_5930667825034166272_n
34847723_1886232668083301_6010100998905790464_n
Baadhi ya Wananchi wa kijiji hicho wamekumbwa na taharuki kuhofia usalama wa maisha yao kwa matukio hayo ya vifo na nyumba kuungua wakiomba vyombo vya usalama kufika kuimarisha amani na utulivu.
34861221_1886232641416637_3943559857889607680_n
 Jeshi la Polisi wilayani Ngara limethibitisha kutokea kwa matukio hayo ambapo mkuu wa wilaya ya Ngara Luteni Kanali Michael Mtenjele amewataka Wananchi kuishi kwa amani na utulivu na kwamba serikali haiamini kuwepo vitendo vya ushirikina.


Na -Shaaban Ndyamukama-Ngara.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad

Contact Form

Name

Email *

Message *