Bunge la Tanzania Kujenga Vyoo vya Kisasa kwa Wanafunzi wa Kike nchi Nzima. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Friday, June 08, 2018

Bunge la Tanzania Kujenga Vyoo vya Kisasa kwa Wanafunzi wa Kike nchi Nzima.

Choo cha Kisaa cha Wanafunzi Katika Shule ya Msingi Mtamaa Manispaa Ya Singida mkoani Singida.

 Picha na Maktaba yetu.
Choo cha Wasichana.

Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Job Ndugai amesema watahakikisha wanajenga vyoo vya mfano katika  kila halmashauri kote nchini kwa wanafunzi wasichana na watu wenye mahitaji maalumu ili waepukane na changamoto zinazowakabili.

Spika Ndugai amesema hayo bungeni Dodoma alipozungumza na waandishi wa habari ambapo amesema kwa sasa wataanza kukusanya fedha za ujenzi huo kupitia zoezi la kuosha magari .

Kwa mujibu wa Spika Ndugai zoezi hilo litahusisha wabunge wote pamoja na mawaziri ili kufikia lengo lililokusudiwa. 
Choo bora katika Shule ya Msingi Unyankindi Manispaa ya Singida kilichojengwa na shirika la SEMA la mkoa wa Singida.

Katika hatua nyingine, Walimu Wakuu wa Shule za Msingi mbalimbali Nchini wamekutana na kufanya kongamano lenye lengo la kuweza kuboresha taaluma zao wakiwa kama Walezi wa Watoto Wanafunzi wawapo Shuleni sambamba na kujadiliana na mabadiliko ya ufundishaji kwa njia ya kisasa zaidi.

Kongamano hilo limefanyika jijini Dar es Salaama ambapo limekutanisha Walimu Wakuu wa Shule za Msingi zaidi ya 200 wengi wakiwa Wakuu wa Shule za Msingi binafsi ambapo wampatiwa mada zenye kujenga taalum yao kulingana na wanafunzi wanaowafundisha.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad