Baadhi ya
wagonjwa wakiandaliwa kwa safari ya
Bugando Mwanza eneo la Uwanja wa ndege Ruganzo,wilayani Ngara mkoani Kagera.
|
Afisa
mwandamizi wa Shirika la kuhudumia wakimbizi UNHCR wilayani Ngara Bi. Irene
Babu.
Idadi ya
vifo vya Wakimbizi waliopata ajali kwenye mteremko wenye kona kali wa K9 katika
kijiji Kasharazi wilayani Ngara mkoani Kagera, imeongezeka na kufikia 8 baada
ya wawili kufariki wakipatiwa matibabu katika Hospitali ya Murugwanza na mmoja
katika hospitali ya Nyamiaga.
|
Majeruhi wote waliopata rufaa wamekwishasafirishwa kwa ndege ya
UNHCR kwenda hospitali ya Bugando kupitia uwanja wa ndege wa Ruganzo uliopo
wilayani Ngara
|
![]() |
Mganga Mkuu
wa Hospitali ya Murugwanza ya Wilayani Ngara Dr. Remmy Andrew amesema katika Hospitali hiyo alipokea Majeruhi 65
kati yao 30 ni Wanawake na 35 ni Wanaume
na kwamba waliotibiwa na kuruhusiwa ni 40 na waliopatiwa rufaa kwenda Hospitali
ya Bugando ni 7
Aidha Mganga
Mfawidhi wa Hospitali ya Nyamiaga Dr.
Simon Kyamwenge amesema Hospitali hiyo ilipokea Majeruhi 31 kati yao Wanaume
ni 24 na Wanawake 7 na kwamba mpaka sasa ameruhusiwa mtu mmoja pekee.
Pia Dr. Kyamwenge amesema Majeruhi 12 wenye
hali mbaya wamepewa rufaa ya kupelekwa katika Hospitali ya Bugando Jijini
Mwanza kwa matibabu zaidi.
Habari/Picha kwa Hisani ya RADIOKWIZERA.CO.TZ
|
No comments:
Post a Comment