Simba SC
imeshinda kwa mabao 4-0 dhidi ya Singida United katika mechi hiyo ilikuwa
inasubiriwa kwa hamu kubwa na mashabiki wa soka nchini.
Mchezaji
Said Hamis Ndemla alitengeneza mabao mawili moja akifunga Emmanuel Okwi na
jingine Asante Kwasi.
Mwenyekiti
wa Kamtai ya Usajili ya Simba, Zacharia Hans Poppe ametoa zawadi ya gari kwa
mchezaji huyo wa Simba SC, Said Hamis Ndemla.
Hans Poppe
ametangza kumpa Ndemla gari baada ya kuonyesha kiwango kizuri cha kuvutia
katika mechi dhidi ya Singida United, Jana January 18,2018.
“Nilikuwa nikimfuatilia kama ambavyo nimekuwa
nikisema nahitaji mchezaji mwenye nidhamu na ambaye hawezi kubadilika. Utaona
Ndemla amekuwa benchi lakini akiingia uwanjani anaonyesha mchango wake,”
alisema.
“Tena pamoja
na kukaa benchi, hakuwahi kuonyesha utovu wa nidhamu. Badala yake kila akipata
nafasi amekuwa akijituma na kuisaidia timu.”
Hii ni mara
ya pili Hans Poppe anatoa gari kwa mchezaji wa Simba SC. Alianza na Hussein
Zimbwe aliyempa gari aina ya Toyota Raum. Lakini akaonyesha gari aina ya Toyota
Lactic na kusema atapewa mchezaji atakayefanya vizuri.
Kuhusiana na
aina, leo amesema: “Aina utaijua baadaye ila gari haiko mbali. Hivyo
tutaangalia siku yenye nafasi atakabidhiwa.”
MSIMAMO WA LIGI ULIVYOSASA.
|
No comments:
Post a Comment