Leo September 5, 2017 ni tarehe maalumu ya kuanza kwa Mkutano
wa Nane wa Bunge la 11.
Taarifa kutoka Ofisi ya Bunge Dodoma hapo Jana September 4,
2017 ni kwamba ratiba rasmi ya mambo yote makubwa yatakayofanyika kwa kipindi
chote wakati Bunge likiendelea.
Taarifa imesema…
Mkutano wa Nane wa Bunge unatarajiwa
kuanza kesho Jumanne tarehe 5 Septemba, 2017 na kumalizika tarehe 15 Septemba
2017 Mjini Dodoma. Shughuli zilizopangwa kufanyika katika Mkutano huo ni kama
ifuatavyo:-
- KIAPO CHA UAMINIFU
Kutakuwa na Kiapo cha Uaminifu kwa
Waheshimiwa Wabunge saba wa Chama cha Wananchi (CUF) walioteuliwa na Tume ya
Taifa ya Uchaguzi hivi karibuni. Wabunge hao wapya watakaoapishwa ni:-
- Mhe. Alfredina Apolinary Kahigi
- Mhe. Kiaza Hussein Mayeye
- Mhe. Nuru Awadhi Bafadhili
- Mhe. Rukia Ahmed Kassim
- Mhe. Shamsia Aziz Mtamba
- Mhe. Sonia Jumaa Magogo
- Mhe. Zainab Mndolwa Amir
- MISWADA YA SERIKALI
Katika Mkutano huu wa Nane wa Bunge
jumla ya Miswada mitatu inatarajiwa kusomwa kwa hatua zake zote.
Miswada hiyo ni :-
- Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria Mbalimbali
Na. 3 wa Mwaka 2017 (The Written Laws (Miscellaneous Amendments)
(No. 3) Bill, 2017)
- Muswada wa Sheria ya Reli wa Mwaka 2017 (The
Railways Bill, 2017)
- Muswada wa Sheria ya Madaktari, Madaktari wa Meno na
Wataalam wa Afya Shirikishi wa Mwaka 2016 (The Medical, Dental
and Allied Health Professionals Bill, 2016)
Aidha, Katika Mkutano huu wa Bunge
Maazimio matano yanatarajiwa kuridhiwa. Maazimio hayo ni:-
- Azimio la Bunge la Kuridhia Itifaki ya Jumuiya ya
Afrika Mashariki ya Afya ya Mimea, Usalama wa Wanyama na Chakula (The
East African Community Protocol on Sanitary and Phytonisanitary (SPS)
Measures).
- Azimio la Bunge la Kuridhia Itifaki ya Amani na Usalama
wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (East African Community Protocol on
Peace and Security.
- Azimio la Bunge la Kuridhia Mkataba ya kuanzisha
Kamisheni ya Pamoja kati ya Tanzania na Malawi kuendeleza Bonde la Mto
Songwe (Convection of Establishment of Joint Songwe River Basin
Commission between Tanzania and Malawi).
- Azimio la Bunge la Kuridhia Mkataba (Intergovernmental
Agreement – IGA) baina ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania na Serikali ya Jamhuri ya Uganda kuhusu Mradi wa Ujenzi wa bomba
la kusafirisha mafuta ghafi la Afrika Mashariki. (East Africa
Crude Oil Pipeline – EACOP) kutoka Hoima (Uganda) hadi Tanga
(Tanzania).
- Azimio la Bunge la Kuridhia Itifaki ya Nyongeza ya Tisa
ya Mwaka 2016 ya Katiba ya Umoja wa Posta Duniani.
- TAARIFA YA KAMATI
Bunge pia linatarajia kupokea
Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Sheria Ndogo kuhusu uchambuzi wa Sheria Ndogo.
- MASWALI
Katika Mkutano huu jumla ya maswali
ya kawaida 125 yanatarajiwa kuulizwa na kujibiwa Bungeni. Aidha, kwa mujibu wa
Kanuni ya 38 (1) ya Kanuni za Kudumu za Bunge wastani wa maswali 16 ya papo kwa
papo kwa Mheshimiwa Waziri Mkuu yataulizwa na kujibiwa pia siku za Alhamisi.
- TAARIFA ZA KAMATI MAALUM
Katika Mkutano wa Saba wa Bunge la
Kumi na Moja Mheshimiwa Spika aliunda Kamati Maalum mbili (2)
kwa ajili ya kuchunguza biashara ya Madini aina ya Tanzanite na Almasi.
Kamati hizo zilizopewa siku 30 zimekamilisha kazi hiyo na zitawasilisha taarifa
zao keshokutwa tarehe 6 Septemba 2017 katika hafla fupi
itakayofanyika katika viwanja vya Bunge na kuhudhuriwa na viongozi wa Kitaifa.
Katika tukio hilo, Mhe. Spika atapokea taarifa hizo na kuzikabidhi kwa Mhe.
Waziri Mkuu.
Matangazo ya hafla hiyo yatarushwa moja kwa moja katika Channel ya
Bunge.
|
No comments:
Post a Comment