Halmashauri
za Wilaya zimechangia kiasi cha shilingi 499,782,895 sawa na asilimia 3% Aidha
wananchi wamechangia shilingi 8,441,593,693 sawa na asilimia 46% Wahisani
wamechangia shilingi 5,178,273,867 sawa na asilimia 26%.
Mwenge wa
Uhuru mwaka huu (2017) umebeba kaulimbiu isemayo “Shiriki Kukuza Uchumi wa
Viwanda kwa Maendeleo ya Nchi yetu.” Kauli mbiu hii inawahamasisha wananchi
hususani wa Mkoa wa Kagera kushiriki kikamilifu katika shughuli za
kuichumi ambazo zinatoa fursa za kuanzisha na kutumia viwanda katika kusindika
mazao na bidhaa mbalimbali zinazopatikana katika mkoa wetu ili kukuza uchumi
wetu kwa maendeleo ya Mkoa na Taifa letu kwa ujumla.
|
Mara baada
ya kupokea Mwenge huo wa Uhuru Mkuu wa Mkoa wa KageraMhe. Kijuu
alimkabidhi Mkuu wa Wilaya ya Biharamulo Mhe. Saada Malunde na Mwenge wa Uhuru
ukaanza mara moja mbio zake wilayani humo za kukagua miradi ya maendelo ambapo
moja ya miradi iliyokaguliwa na Kiongozi wa mbio za Mwenge Amour Hamad Amour ni
kituo cha Afya cha Nemba chenye thamani ya shilingi milioni 66.
|
Mwenge wa
Uhuru ukiwa Mkoani Kagera Agosti 2, 2017 umekabidhiwa Wilayani Ngara
na kuendelea mbio zake Wilayani humo.
Ukiwa wilayani
Ngara, Mwenge wa Uhuru utapitia miradi 11 ya Maendeleo yenye thamani
ya Tsh4.5 Bilioni kabla ya kuingia wilaya ya Karagwe, Kyerwa, Misenyi, Halmashauri ya Bukoba , Manispaa ya Bukoba na kuhitimisha mbio zake Kimkoa wilayani Muleba.
|
No comments:
Post a Comment