Mbunge wa
Hai, Freeman Aikaely Mbowe, mfanyabiashara mkubwa nchini, Yusuf Manji na
Mchungaji Josephat Gwajima wametajwa kwenye orodha ya pili ya Mkuu wa Mkoa wa
Dar es Salaam, Paul Makonda ya watu mashuhuri wanaohusishwa kwenye biashara ya
madawa ya kulevya.
Makonda
amemtaja pia Mbunge wa zamani wa Kinondoni, Iddi Azan na mfanyabiashara maarufu
wa nguo, Hussein Pambakali kwenye orodha hiyo.
Ameielezea
orodha hiyo kuwa ni ya wale ambao wanahisishwa na biashara hiyo haramu na
wengine wana taarifa muhimu zinazoweza kuwasaidia polisi kuwatia nguvuni vinara
wa biashara hiyo.
Watu hao
watahojiwa na Polisi kama ilivyofanyika kwa watu waliotajwa kwenye orodha ya
kwanza iliyohusisha pia mastaa wa muziki na filamu.
Wengine wanaohitaji ni pamoja na wamiliki wa Slipway na Yatchy Club.
Orodha ya
awamu ya pili ya Makonda ina jumla ya majina 65.
Makonda amewataka
watu wote 65 waliotajwa, kuhakikisha wanaripoti kwenye Kituo Kikuu cha Polisi
Dar es Salaam (Sentro) siku ya Ijumaa saa 5 asubuhi kwa mahojiano zaidi.
Akizungumza
na wanahabari ofisini kwake, Makonda amesema kuwa, waliokamatwa awali ndiyo
waliofanikisha kupatikana kwa orodha hiyo mpya.
|
No comments:
Post a Comment