Rais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt John Pombe Magufuli ametoa wito kwa wakazi
wa maeneo mbalimbali nchini kutumia mvua zinzoendelea kunyesha kwaajili ya
kulima mazao yanayostahimili ukame baada ya kutegemea chakula kutoka
serikalini.
Hayo
ameyazungumza alipowasili eneo la Busisi wilayani Sengerema mkoani Mwanza
kutokea Chato mkoani Geita huku akipokelewa na kamati ya ulinzi na usalama ya
Mwanza wakiongozwa na mkuu wa mkoa.
“Ninafahamu
wapo wanasiasa wachache ambao wanafikiri mzee bure, kila kitu kikitokea
serikali ifanye, serikali ninayoiongoza mimi haitatoa kitu, mlinichagua
niwaeleze ukweli na mimi nawaeleza ukweli,” alisema Magufuli.
“Sasa hivi
wakati wa kulima mahindi umebadilika, tusijilazimishe kulima mahindi ambayo
yanahitaji mvua nyingi mvua zinaponyesha tulime, na asiye fanya kazi na asile,
msije kamwe mkadanganywa na mtu yeyote kwamba patakuwa na chakula cha serikali
nataka niwaambie hakuna shamba la serikali,” alisema.
“Nani
anaweza akanionyesha shamba la serikali, hakuna shamba la serikali, mlinichagua
niwaambie ukweli na ukweli utabaki kuwa ukweli ni lazima tufanye kazi
tujipange,” aliongeza
|
No comments:
Post a Comment