![]() |
Hali
kadhalika ilianzisha safari za Kimataifa
kwenda Entebbe nchini Uganda, Nairobi Kenya, Harare Zimbabwe, Johannesburg Afrika Kusini
na Lusaka nchini Zambia katika kipindi cha miaka mitatu ya kuendesha shughuli
zake.
“Tangu
tuanze safari zetu tumeshabeba abiria
zaidi ya 1,800,000 ambapo utafiti wetu unaonesha kuwa zaidi ya theluthi moja ya abiria wetu walikuwa ndio mara yao ya
kwanza kumudu kusafiri kwa ndege”,
anasema Corse.
Aliendelea
kusema, “kuongeza ndege nyingine kwenye safari zetu kunatupa fursa muhimu ya kuongeza masafa kwa njia zetu zilizopo ili kukidhi mahitaji ya wateja, na na
inasaidia kwenye lengo letu la kuongeza njia moja ya kimataifa kwenye mtandao
wetu kwa mwaka huu 2016”.
Hali
kadhalika, Corse anabainisha kuwa ndege hiyo mpya inamanisha kuwa fastjet ni sawia na ni kubwa
katika kutosheleza kupanuka kwa shughuli za fastjet.
Ndege hiyo
A319 ambayo ni Airbus ni ya injini mbili ambazo zinatoa kiwango cha juu cha ufanisi
pamoja na kiwango cha chini kabisa cha madhara kwenye mazingira, ikiwa ni
nyongeza kwenye viwango vya juu vya hali
ya kuliwaza ndani ya ndege hiyo ya kisiasa.
Ndege hiyo
ina uwezo wa kubeba abiria 156 ambaop wanamudu viwango vya chini vya
kuendesha mtindo wa maisha wa gharama nafuu ambao unaendeshwa na Fastjet
Tanzania.
Baadhi
ya njia muhimu ambazo ndege hiyo mpya
itakuwa inahudumia ni njia mpya iliyoanzishwa
hivi karibuni kati ya Dar es Salaam na Nairobi, Kilimanjaro na Nairobi na Dar es Salaam kwenda Zanzibar ambazo zote
zilianza kwa mara ya kwanza Januari 11, 2016. njia hizi mpya zote ni kielelezo muhimu muda mrefu kwenye
upanuzi wa njia za fastjet kitaifa na
kimataifa.
Fastjet
inatarajia kuongeza ndege zaidi kwenye njia yake ya Kenya kutokana na mahitaji ya wateja kuongezeka
kunakosababisha na kumudu, usalama, kasi na huduma kwa wakati, na hali
kadhalika imeshajionesha kuwa kuna
matarajio ya kuzindua safari kati ya Zanzibar na Nairobi na hali kadhalika kati ya Dar es Salaam na
Mombasa baadaye mwaka 2016.
“Usafiri wa
anga unaoumudu ni muhimu kwenye kukuza
uchumi wa Tanzanoa, hususani kwenye
kukuza sekta za biashara na utalii”, alisema Corse.
Hali
kadhalika Corse alibainisha kuwa ndege hiyo mpya inamaanisha kwamba ndege za
Fastjet zitatosheleza kiasi cha kutosha kusaidia kwenye changamoto za usimamizi
na uendeshaji iwapo ndege moja miongoni mwake itakuwa haifanyi
kazi au kama ipo kwenye matengenezo au ukarabati wa lazima.
|
Post Top Ad
Tuesday, February 02, 2016

UCHUMI NA BIASHARA:-fastjet yaongeza ndege ya tano .
Tags
# DONDOO
# MATUKIO
Sambaza Hii
Chief Editor | Mhariri
Journalist / Chief Editor / Tanzanian Blogger
Simu: 0756830214 / 0620197747 / 0789925630.
Makala Inayofuata
UBINADAMU WETU:-Mfuko wa Dharura wa UN watoa Dola Milioni 11 kusaidia wakimbizi wa Burundi na Jamii ya Tanzania.
Makala Iliyopita
BUNGENI DODOMA LEO:- Shillingi Billioni 233 zatengwa kuajiri Vijana 71,408 ikiwemo Kada ya Afya na Waalimu.
Muonekano wa Uwanja wa CCM Kirumba Jijini Mwanza.
AnonymousDec 10, 2019Viongozi Wilayani Kasulu watakiwa Kuimarisha Usalama Katika Korongo la Bolelo.
AnonymousJun 29, 2019Shirika la Ndege la Tanzania Laanza Safari za Afrika Kusini Leo 28/06/2019.
AnonymousJun 28, 2019
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment