Mrimi
Zabloni (Katikati) ambae ni Katibu wa Mbunge wa Jimbo la Tarime Vijijini
akiongea na wanahabari.
|
Kulia ni
Mwl.Chacha Heche ambae ni Katibu wa Chadema Mkoani Mara akiongea na wanahabari
nje ya Mahakama Kuu Kanda ya Mwanza.
Na:George
Binagi.
MAHAKA kuu
Kanda ya Mwanza jana imeitupilia mbali kesi ya kupinga matokeo ya Uchaguzi Mkuu
uliofanyika Novemba 25 mwaka jana 2015, katika Jimbo la Tarime Vijijini Mkoani
Mara, iliyofunguliwa na aliekuwa mgombea ubunge katika jimbo hilo kupitia Chama
cha Mapinduzi CCM,Christopher Ryoba Kangoye.
Katika kesi
hiyo,wajibu maombi walikuwa ni Mbunge wa Jimbo la Tarime Vijijini Mhe.John
Heche (CHADEMA), Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Tarime pamoja na
Mwanasheria Mkuu wa Serikali ambapo mtoa maombi alikuwa akiiomba Mahakama
kutengua matokeo ya Uchaguzi Mkuu katika Jimbo hilo kwa kuwa haukuwa huru na
haki.
Baada ya
Mahakama hiyo kupitia kwa Jaji Lameck Mlacha kusikiliza utetezi wa pande zote,
iliamua kuifuta kesi hiyo ambayo ilikuwa ni nambari nne ya mwaka 2015 kutokana
na hoja za mleta maombi kuwa na kasoro mbalimbali ikiwemo kutoainisha majina ya
waliokuwa wakilalamikiwa kuvuruga uchaguzi Jimboni humo.
Wakili wa
mleta maombi Costantine Mutalemwa pamoja na Wakili wa mjibu maombi Paul Kipeja aliekuwa
akisaidiana na Wakili Tundu Lisu katika kesi hiyo, wameelezea kuridhika na
maamuzi ya Mahakama hiyo..Kusoma
zaidi bofya HAPA.
|
No comments:
Post a Comment