Waziri wa
Habari,Utamaduni, Wasanii,na Michezo
Nape Nnauye akitoa kauli Bungeni
mjini Dodoma Januari 27, 2016.
Hapo majira
ya Asubuhi,Mwenyekiti wa Bunge, Andrew Chenge aliahirisha bunge mara mbili
kutokana na mvutano ulioibuka baada ya Mbunge wa Kigoma Mjini, Zitto Kabwe
kuomba bunge liahirishe kujadili hotuba ya rais na badala yake wajadili kuzuiwa
kwa Shirika la Utangazaji la Tanzania (TBC) kurusha matangazo ya moja kwa moja.
Kabla ya
kuahirishwa kwa bunge, Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape
Nnauye aliwasilisha taarifa ya serikali kulieleza bunge kwamba, serikali
imesitisha huduma ya matangazo ya moja kwa moja kupitia TBC.
Kutokana na
taarifa hiyo, Zitto alisimama na kuliomba bunge kusitisha shughuli za kuendelea
kujadili hotuba ya rais ambayo ilianza kujadiliwa jana ili kutoa fursa
kujadiliwa hatua ya serikali kuzuia haki ya wananchi kupata matangazao ya moja
kwa moja kupitia televisheni hiyo.
Hata hivyo,
Chenge alianza kuonesha nia ya kutaka kuzima hoja ya Zitto lakini wabunge wa
upinzani kwa umoja wao waliungana na Zitto katika kushikilia msimamo wa
kujadiliwa suala la TBC kabla ya kuendelea na mjadala wa hotuba ya rais.
Yalisikika
maneno kama ‘usituburuze, mtemi, hapa hakuna kuburuzana’ huku wabunge wengine
wakipiga kelele kuashiria kuunga mkono hoja ya Zitto.
Kutokana na
mvutano huo, Chenge alilazimika kuagiza kamati ya uongozi kukutana ili kujadili
taarifa hiyo na baadaye kuwasilisha kulichojadiliwa na kamati hiyo.
“Naipa
kamati saa moja,” alisema Chenge jambo ambalo lilipokelewa kwa mikono miwili na
upinzani. Baada ya kauli hiyo mwenyekiti huyo aliahirisha bunge kwa saa moja.
Hata hivyo,
baada ya bunge hilo kurejea tena baada ya kupita saa moja , Chenge aliahirisha
tena bunge kwa kuwa, kamati ilikuwa haijamaliza kujadili.
Wakati
akizungumza bungeni wakati wa kuwasilisha kauli ya serikali Nape alisema,
“naomba kutoa kauli ya serikali kuhusu TBC kutangaza moja kwa moja vikao vya
majadiliano ya bunge.”
TBC ilianza
kurusha moja kwa moja matangazo ya vikao vya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania mwaka 2005. Kabla ya kuanza kurusha moja kwa moja, TBC wakati huo
televisheni ya taifa ilikuwa inarekodi matukio yote ya bunge na kurusha usiku
katika vipindi maalumu vilivyojulikana kama bungeni leo kwa maana ya yaliyojiri
ndani ya bunge kwa siku husika.
Hata hivyo
Nape alisema “baada ya kuanza kwa utaratibu wa kuanza kurusha matangazo moja
kwa moja mwaka 2005, gharama za kufanya kazi hio zimekua zikipanda kwa kasi
hadi kufikia Sh. 4.2 bilioni kwa mwaka kwa maana ya mikutano minne ya bunge.
“Shirika
limekuwa likigharamia kwa sehemu kubwa matangazo hayo kwa kutumia mapato yake
yanayotokana na matangazo madogo madogo ya biashara, ifahamike kuwa asilimia 75
ni vipindi vingi vinavyolenga kutoa elimu kwa umma na asilimia 25 ni burudani.”
Nape
amesema, kutokana na hali hii, TBC imeona ni busara kubadilisha mfumo wa
utangazaji wa shughuli za bunge ili kukabiliana na kupanda kwa gharama za
uendeshaji.
Amesema TBC
imeona ni busara kuanzia mkutano huu wa bunge iwe inarusha baadhi ya matangazo
ya bunge moja kwa moja yaani ‘live’ ikiwa ni njia ya kubana matumizi.
Amefafanua
kuwa, “chini ya utaratibu huu, TBC itahakikisha kuwa, baadhi ya matukio ya
matukio ya bunge yatarushwa moja kwa moja na mengine kurekodiwa na kuandaliwa
kipindi maalum kitakachoitwa leo katika bunge.
“Kipindi
hiki kitakua na mambo yote muhimu yaliyojiri ndani ya bunge kwa siku husika.
Kipindi hichi kitakuwa kinarushwa kuanzia saa nne usiku hadi saa tano usiku.”
HAPA CHINI TAZAMA VIDEO KWA KUBOFYA PLAY.
|
Wednesday, January 27, 2016
Home
HABARI
SIASA
LEO JAN 27,2016 BUNGENI DODOMA:-Serikali Yatoa Ufafanuzi Juu Ya Kutorusha Matangazo Ya Bunge.
LEO JAN 27,2016 BUNGENI DODOMA:-Serikali Yatoa Ufafanuzi Juu Ya Kutorusha Matangazo Ya Bunge.
Tags
# HABARI
# SIASA
Sambaza Hii
Chief Editor | Mhariri
SIASA
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Kuhusu Mwandishi
Journalist / Chief Editor / Tanzanian Blogger
Simu: 0756830214 / 0620197747 / 0789925630.
No comments:
Post a Comment