Ofisa
 Miradi ya Mawasiliano, Habari na Tehama wa Shirika la Kimataifa la 
Sayansi, Elimu na Utamaduni (UNESCO) nchini, Al Amin Yusuph, akizungumza
 katika kongamano lililowakutanisha watendaji kutoka Redio za jamii 
nchini katika mji wa Terat, wilayani Simanjiro mkoa wa Manyara jana.
Mwenyekiti
 wa Muungano wa Redio za Kijamii nchini (COMNETA), Sekiku Joseph 
akizungumza katika Kongamano hilo ambalo amesisitiza umuhimu wa viongozi
 wa Radio za kijamii kuthamini michango inayotolewa na wafadhili ili 
iweze kuwa endelevu.
Mshauri
 na Mkufunzi wa masuala ya vyombo vya habari jamii kutoka Shirika la 
Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) Bi. Rose Haji 
Mwalimu akisistiza jambo katika mafunzo hayo.
Afisa Miradi mpya wa Unesco, Nancy Kaizirege akisisitiza jambo.
Mkurugenzi
 wa Redio ya Jamii Uvinza FM, Ayub Kalufya akichangia mada na kuomba 
Unesco kuendelea kutoa usaidizi kwao kutokana na mchango wanaoutoa kwa 
jamii.
Afisa
 Miradi mpya wa Unesco, Nancy Kaizirege akisisitiza jambo wakati mafunzo
 hayo yakiendelea. kulia ni Meneja wa Orkonerei Radio Service Simanjiro 
Manyara (ORS FM), Bw.Baraka Ole Maika.
Mwenyekiti
 wa Bodi ya Redio ya Jamii 94.9 FM , Mkoani Pemba, Hamidu Hassan Bakari 
akizungumza namna Redio yake itakavyonufaika kupitia mafunzo ya 
kuwajengea uwezo na vifaa ya matangazo.
Meneja wa Redio Kahama FM, Marco Mipawa, akizungumza jambo.
Mwandishi Wetu,Simanjiro
Shirika
 la Umoja wa Mataifa la Elimu,Sayansi na Utamaduni(UNESCO) limeendelea 
kuimarisha Redio za Jamii nchini kwa kuwapa mafunzo ya mara kwa mara 
watendaji wa ngazi mbalimbali kwa lengo la kuzifanya Redio hizo 
kuwahudumia vema wananchi wanaoishi maeneo ya vijijini.
Ofisa
 Miradi ya Mawasiliano, Habari na Tehama wa Shirika la Kimataifa la 
Sayansi, Elimu na Utamaduni (UNESCO) nchini, Al Amin Yusuph amesema 
kumekuwa na mafanikio tangu mradi huo kuanza miaka mitatu iliyopita 
chini ya ufadhili wa UNESCO, Shirika la Maendeleo la Sweden (SIDA) na 
Serikali ya Uswizi ambapo licha ya kuwajengea uwezo vifaa vya 
kieletroniki vilitolewa kwa Redio hizo.
 Kongamano
 hilo la mwaka la siku tatu(3) linafanyika katika Kituo cha Orkonerei 
Radio Service Simanjiro Manyara (ORS), Terat wilayani Simanjiro mkoa wa 
Manyara na limewaleta pamoja watendaji wa Redio za Jamii 20 kutoka mikoa
 mbalimbali ya Tanzania Bara na Zanzibar .
“Tunalenga
 kuwajengea uwezo ili hizi Redio za Jamii zifanye kazi kwa weredi  ya 
kuleta maendeleo endelevu kwa wananchi waweze kushiriki mijadala 
inayohusu sekta za afya, elimu na kilimo,”amesema Yusuph
UNESCO inafanya kazi kwa karibu na Muungano wa Radio za Kijamii Tanzania(COMNETA)unaongozwa na Mwenyekiti wake Sekiku Joseph.
Papo kwa Papo >>>> Pata Picha, Habari za  Siasa, Kijamii, Biashara, Muziki na Michezo na Nyingine kwa kujiunga  na mimi hapa…..FACEBOOK , TWITTER , INSTAGRAM , Pia tutumie tukio la Picha kwa WhatsApp +255789925630.     





No comments:
Post a Comment