JIMBO LA KARAGWE
Mgombea
Ubunge wa Jimbo la Karagwe Mkoani Kagera kupitia Chama cha Mapinduzi Bw
Innocent Bashugwa ametangazwa kuwa mshindi ambapo akitangaza matokeo ya
uchaguzi huo Msimamizi wa Uchaguzi wilayani Karagwe Bw Richard Ruyango
amesema Bw Bashungwa amewashinda wagombea watatu kutoka Chadema, TLP na
UDP baada ya kupata kura elfu 57 na 322 sawa na asilimia 54.92
Kwa upande
wake Bw
Bashungwa amewashukuru wakazi wa Karagwe kwa kumuamini na ambapo
ameahidi kuwatumikia kikamolifu kwa kutekeleza vipaumbele vyakeikiwemo Elimu,
Afya na Barabara
JIMBO LA KIGOMA
Mgombea
Ubunge wa Jimbo la Kigoma Mjini kupitia Chama cha ACT Wazalendo Bw
Zitto Kabwe ametangazwa kuwa Mshindi wa nafasi hiyo
Akitangaza
matokeo ya Uchaguzi uliofanyika jana October 25,2015, Msimamizi wa Uchaguzi
katika Manispaa hiyo Mhandisi Bonipace Nyambele amesema
jimbo hilo mgombea huyo ameshinda nafasi hiyo iliyokuwa ikiwaniwa na wagombea
kumi na sita jimboni humo
Mhandisi Nyambele amesema Bw Zitto amepata kura
Elfu 31 na 546 kati ya kura Elfu 91 na 824 zilizopigwa.
Bw Kabwe
amefuatiwa na Dr Aman Kaburu kupitia CCM aliyepata kura Elfu 17 na 314 huku
Bw Daniel Lumenyera kupitia Chadema kipata Kura Elfu 12 na 77
Bw Zitto Kabwe amesema atahakikisha anafanya kazi
kwa maslahi ya wananchi na kulifanya jimbo hilo kuwa mfano kimaendeleo hapa
nchini
JIMBO LA KAHAMA
Mgombea wa
Ubunge wa Jimbo la Kahama Mjini kupitia Chama cha Mapinduzi Bw
Jumanne Kishimba ametangazwa kuwa Mshindi dhidi ya Bw James Lembeli wa Chama
cha Demokrasia na Maendeleo, Chadema
Msimamizi wa
uchaguzi katika Jimbo la Kahama Mjini Bw Anderson Msumbwa amesema Bw
Kishimba ameshinda kwa kura Elfu 47 na 555 akifuatiwa na Bw
Lembeli aliyepata kuta elfu 30 na 122
huku Bw Bobson Wambura awa ACT Wazalendo akipata Kuta 605
Amesema
katika Jimbo la Kahama mjini lililokuwa na wapiga Kura Laki Moja Elfu 49 na 344
waliokuwa wamejiandikisha huku watu elfu 78 na 280 wakijitokeza kupiga kura,
hakukuwa na kura iliyoharibika.
Bw Msumbwa
amesema katika uchaguzi huo jimbo la Kahama mjini lilikuwa na vituo 321 vya
kupigia kura katika kata 20 na kwamba katika matokeo ya udiwani, Chama cha
Mapinduzi kimepata madiwani 19 na Chadema kimepata kiti kimoja.
Papo kwa Papo >>>> Pata Picha, Habari za Siasa, Kijamii, Biashara, Muziki na Michezo na Nyingine kwa kujiunga na mimi hapa…..FACEBOOK , TWITTER , INSTAGRAM , Pia tutumie tukio la Picha kwa WhatsApp +255789925630.
|
No comments:
Post a Comment