MUFTI MPYA WA TANZANIA:-Ni Sheikh Abubakary Zubeir. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Thursday, September 10, 2015

MUFTI MPYA WA TANZANIA:-Ni Sheikh Abubakary Zubeir.

Sheikh-Abubakar-Zuberi-bin-Ally
Mufti mpya wa Tanzania, Sheikh Abubakary Zubeir.

Wajumbe 310 wa Baraza Kuu la Waislamu nchini (Bakwata), leo September 10,2015 wakiwa mkoani Dodoma wamemchagua Sheikh Abubakary Zubeir kuwa Mufti wa Tanzania akiziba nafasi iliyoachwa na hayati Issa Shaaban bin Simba.

 Kabla ya uchaguzi huo, Sheikh Abubakary Zubeir, alikuwa Kaimu Mufti wa Tanzania kwa kipindi cha mpito baada ya kifo cha Sheikh Mkuu, Issa Shaaban bin Simba.

Awali Sheikh Zubeir alikuwa Naibu Mufti wa Sheikh Mkuu na pia Mjumbe wa Baraza Kuu la Ulamaa nchini.

Papo kwa Papo >>>> Pata Picha, Habari za  Siasa, Kijamii, Biashara, Muziki na Michezo na Nyingine kwa kujiunga  na mimi hapa…..FACEBOOK , TWITTER INSTAGRAM , Pia tutumie tukio la Picha kwa WhatsApp +255789925630.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad