TASWIRA PICHA:-Mapokezi ya Ester Bulaya na James Lembeli Jimboni Bunda Jana July 23, 2015. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Friday, July 24, 2015

TASWIRA PICHA:-Mapokezi ya Ester Bulaya na James Lembeli Jimboni Bunda Jana July 23, 2015.

Msafara wa bodaboda uliowapokea Mh Esther Bulaya na Mh James Lembeli walipofika Bunda hapo Jana Julai 23,2015 kwa ajili ya kuhutubia mkutano mkubwa Jimboni Bunda.


Mh Esther Bulaya akisalimiana na Viongozi wa Chadema Bunda waliokuja kuwapokea.

Mbunge wa Viti Maalumu wa CCM aliyehamia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Ester Bulaya akihutubia mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye Uwanja wa Stendi ya zamani Mjini Bunda mkoani Mara.

Mbunge wa Kahama mkoani Shinyanga, James Lembeli aliyehama kutoka CCM na kujiunga Chadema, akihutubia mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye Uwanja wa Stendi ya zamani ya mabasi Mjini Bunda jana Julai 23,2015.

Umati wa wananchi wa Mji wa Bunda na viunga vyake, wakiwa katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye Stendi ya zamani ya mabasi mjini Bunda jana, uliohutubiwa pia na Mbunge wa Viti Maalumu, Ester Bulaya na mwenzake wa Kahama, James Lembeli waliotoka CCM na kuhamia Chadema.

Pata Picha, Habari za Kisiasa, Kijamii, Kiuchumi na Michezo kila stori inayonifikia wakati  wowote ukijiunga na mimi kwa kubonyeza…..FACEBOOK , TWITTER , INSTAGRAM , Pia tutumie tukio la Picha kwa WhatsApp +255789925630.


No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad