MKUTANO WA ACT KASULU:-Machali akabidhiwa kadi ACT, atoa ya moyoni. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Thursday, July 23, 2015

MKUTANO WA ACT KASULU:-Machali akabidhiwa kadi ACT, atoa ya moyoni.

Kiongozi Mkuu wa Chama cha ACT Wazalendo, Zitto Kabwe (kulia) akimtambulisha kwa wananchi mwanachama mpya wa chama hicho Mbunge wa Kasulu Mjini, Moses Machali katika mkutano wa hadhara uliofanyika mjini Kasulu, mkoani Kigoma Julai 21,2015. Picha na Anthony Kayanda.

  Akizungumza baada ya kukabidhiwa kadi na kiongozi wa ACT - Wazalendo, Zitto Kabwe, Naibu Katibu Mkuu huyo wa NCCR - Mageuzi alisema amejiunga baada ya viongozi wa chama hicho kumhujumu katika harakati zake za kutetea masilahi ya Halmashauri ya Wilaya Kasulu.

Zitto afichua

Akizungumza katika mkutano huo, Zitto licha ya kuwataka wananchi wa Kasulu kujiunga na chama hicho, alisema Machali alishajiunga nao muda mrefu na kwamba alichokuwa anasubiri ni kukabidhiwa kadi. “Tulisema lazima tupate baadhi ya wabunge na viongozi maarufu kutoka vyama vingine, sasa tumeanza na Machali na wengine watafuata,” alisema Zitto.

Viongozi wengine waliojiunga na chama hicho jana ni pamoja na kada wa CCM, Emmanuel Mbwiliza aliyewahi kuwa Diwani wa Kata ya Nyumbigwa hadi mwaka 2010 pia akiwa Mjumbe wa Mkutano Mkuu wa CCM kuanzia 2007 hadi 2012.

Katika mkutano huo pia viongozi wengine wa NCCR kutoka Kasulu Mjini na Kasulu Vijijini walijiunga na ACT huku wakiahidi kupambana kuhakikisha wanashinda katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu.

Baadhi ya wananchi hao walionyesha kumuunga mkono Machali katika harakati zake za kutetea Jimbo la Kasulu Mjini kupitia chama chake kipya wakisema watafanya hivyo kutokana na hulka yake ya kupambana na viongozi wanaoonekana kufuja mali ya umma.


Pata Picha, Habari za Kisiasa, Kijamii, Kiuchumi na Michezo kila stori inayonifikia wakati  wowote ukijiunga na mimi kwa kubonyeza…..FACEBOOK , TWITTER , INSTAGRAM , Pia tutumie tukio la Picha kwa WhatsApp +255789925630.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad