Viongozi wa
Umoja wa Katiba ya Wananchi, UKAWA.
UKAWA
umesema kuwa umeshindwa kumtangaza Mgombea Urais kupitia Umoja huo kutokana na
kutopatikana hadi sasa kwa Mgombea Mwenza kutoka Zanzibar.
|
Mwanasheria
Mkuu wa Chama cha Demokrasia na maendeleo (CHADEMA), Tundu Lissu.
Mwanasheria
Mkuu wa Chadema Bw Tundu Lissu amesema Mgombea Urais kupitia Ukawa
ameshapatikana na kwamba kilichochelewesha kutangazwa kwake ni mgombea Mwenza
ambaye taratibu za kumpata zinafanyika.
Akihutubia
wakazi wa Mji wa Geita, katika viwanja vya Shule ya Msingi Nyankumbu Bw Lissu
amesema mgombea wa Ukawa atajulikana hivi karibuni ndani na nje ya nchi.
Amesema
umoja huo unaoundwa na Chadema, NCCR Mageuzi, CUF na NLD utamtangaza mgombea
wake mara baada ya kupatikana kwa Mgombea Mwenza.
Katibu wa
Chadema, Dk Willibrod Slaa ndiye ambaye anapewa nafasi kubwa ya kupitishwa
kugombea urais kwa tiketi ya Ukawa mbele ya mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim
Lipumba na kada wa NCCR-Mageuzi, Dk George Kahangwa, lakini hadi sasa vyama
hivyo bado vinasita kumtangaza mteule wake.
Awali
Mwenyekiti wa Chadema Mkoani Geita, Bw Alphonce Mawazo amesema wakazi wa Geita
hawana maeneo ya uchimbaji madini licha ya mkoa huo kuwa na Madini mengi
aliyodai kuwa yanawanufaisha wawekezaji.
Source:-Radio Kwizera FM.
Pata
Picha, Habari za Kisiasa, Kijamii, Kiuchumi na Michezo kila stori
inayonifikia wakati wowote ukijiunga na mimi kwa kubonyeza…..FACEBOOK , TWITTER , INSTAGRAM , Pia tutumie tukio la Picha kwa WhatsApp +255789925630.
|
No comments:
Post a Comment