KAGAME CUP 2015:-Azam FC na KCCA hao robo fainali leo July 26,2015 ni Yanga na Al Khartoum [Saa 10 Jioni]. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Sunday, July 26, 2015

KAGAME CUP 2015:-Azam FC na KCCA hao robo fainali leo July 26,2015 ni Yanga na Al Khartoum [Saa 10 Jioni].

Bao pekee lililofungwa na mshambuliaji Ivan Sserunkuma limetosha kuipeleka KCCA hatua ya robo fainali ya michuano ya Kombe la Kagame 2015 baada ya Jana July 25,2015 kutoka kifua mbele kwa bao 1-0 dhidi ya Malakia FC.

Sserunkuma amefunga bao hilo dakika ya 12 akimalizia kwa shuti la mguu wa kushoto krosi iliyotua ndani ya sita kutoka wingi ya kulia.

KCCA sasa itasubiri mshindi wa pili katika Kundi A ambalo lina timu za Al Khartoum , Gor Mahia na Yanga SC ambazo tayari zimeshafuzu inagawa bado zina mechi moja kila moja mkononi.
Wachezaji wa Azam FC wakipongezana baada ya Kipre Tchetche kuipatia timu yao bao la pili.

Mshambuliaji wa Azam FC, Kipre Herman Tchetche ameondoka na mpira baada ya kupiga bao 3 maarufu kama hat trick wakati Azam FC ilipoitandika Adama City ya Ethiopia mabao 5-0 jana July 25, 2015 jioni Katika mechi hiyo ya michuano ya Kombe la Kagame 2015.

 Azam FC ilishatinga robo fainali ya mashindano hayo huku Mabao mengine ya Azam FC iliyomaliza kundi C yalifungwa na Aggrey Morris na kiungo kinda Mudathir Yahya.


Kwa matokeo hayo, Azam FC inamaliza kileleni mwa Kundi C kwa pointi zake tisa ikifuatiwa na KCCA yenye pointi sita ambazo zote zinakwenda Robo Fainali, wakati Adama imemaliza bila pointi na inarejea nyumbani, huku Malakia ya Sudan Kusini iliyomaliza na pointi tatu inaweza kufuzu kama mshindi wa tatu bora. 
RATIBA KAGAME CUP 2015.

Jumapili Julai 26, 2015.

Gor Mahia Vs Telecom [Saa 8 Mchana]

Yanga Vs Al Khartoum [Saa 10 Jioni]

ROBO FAINALI KAGAME CUP 2015.

Jumanne Julai 28, 2015.

APR Vs A3

A1 Vs Mshindi wa tatu Bora

Jumatano Julai 29, 2015

Al Shandy Vs C2

C1 Vs A2

Pata Picha, Habari za Kisiasa, Kijamii, Kiuchumi na Michezo kila stori inayonifikia wakati  wowote ukijiunga na mimi kwa kubonyeza…..FACEBOOK , TWITTER , INSTAGRAM , Pia tutumie tukio la Picha kwa WhatsApp +255789925630.


No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad