AJALI / PICHA:- Watu watano wamekufa papo hapo na wengine 11 wakiwa mahututi, baada ya lori la mizigo Mitsubish Fusso, kuigonga Hiace Wilaya ya Siha mkoani Kilimanjaro. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Saturday, July 18, 2015

AJALI / PICHA:- Watu watano wamekufa papo hapo na wengine 11 wakiwa mahututi, baada ya lori la mizigo Mitsubish Fusso, kuigonga Hiace Wilaya ya Siha mkoani Kilimanjaro.

Basi dogo la abiria (Hiace) T 196 AAW linalofanya safari zake kati ya miji ya Sanya Juu na Moshi mjini likiwa limeharibika vibaya baada ya kugongwa kwa nyuma na lori.

Watu watano wamekufa papo hapo na wengine 11 wakiwa mahututi, baada ya lori la mizigo Mitsubish Fusso, kuigonga Hiace linalofanya safari zake kati ya miji ya Sanya Juu, Wilaya ya Siha na Moshi Mjini, mkoani Kilimanjaro.

 Ajali hiyo iliyotokea jana Julai 17,2015 saa 12:40 asubuhi katika daraja la mto Kikavu, Wilaya ya Hai, iliyahusisha Fusso lenye namba za usajili T 430 AAQ na Toyota Hiace, T 196 AAW lililokuwa linaendeshwa na dereva anayefahamika kwa jina la ‘Baba D’.

Habari zilizopatikana katika eneo la tukio na  kuthibitishwa na Kamanda wa Polisi, Mkoa wa Kilimanjaro (SACP), Fulgence Ngonyani, zinaeleza kuwa chanzo cha ajali hiyo ni mwendo kasi wa dereva wa lori ambaye hata hivyo, alitokomea baada ya kusababisha ajali hiyo.

Alisema baadhi ya majeruhi walikimbizwa katika Hospitali ya Rufaa ya KCMC na wengine walipelekwa Hospitali ya Rufaa ya mkoa wa Kilimanjaro (Mawenzi) kwa matibabu. Kamanda Ngonyani alisema miili ya marehemu imehifadhiwa katika Hospitali ya Mawenzi ikisubiri kutambuliwa na ndugu na jamaa zao.

Hata hivyo, watu walioshuhudia ajali hiyo, waliieleza kwamba, dereva wa lori hilo  aliligonga kwa nyuma basi dogo la abiria katikati ya daraja, wakati akitokea katika mji mdogo wa Kwa Sadala na kusababisha vifo hivyo.

Grayson Kweka, mkazi wa Kwa Sadala, wilayani hapa alisema, “Huyu dereva wa Fusso alikuwa amepakia mchele na alikuwa akielekea Moshi Mjini, alipofika karibu na daraja la mto Kikavu, lori lilimshinda kutokana na mwendo kasi aliokuwa nao na hivyo kuigonga Hiace na kuua abiria watano papo hapo, akiwamo kondakta wa basi hilo.”

Afisa habari na mahusiano wa KCMC, Gabriel Chisseo aliiambia NIPASHE kuwa walipokea majeruhi saba wa ajali hiyo, wakiwa katika hali mbaya na kulazimika kuingizwa katika chumba maalum cha upasuaji.

Aliwataja majeruhi waliolazwa hospitalini hapo kuwa ni Haji Mdangiwa, Fred Urassa, Levina Mnyampanda, Jenista Unonu, Antonia Msaki, Hawa Hamis na Julieth Massawe.

Pata Picha, Habari za Kisiasa, Kijamii, Kiuchumi na Michezo kila stori inayonifikia wakati  wowote ukijiunga na mimi kwa kubonyeza…..FACEBOOK , TWITTER , INSTAGRAM , Pia tutumie tukio la Picha kwa WhatsApp +255789925630.


No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad