|
NGARA.
Matokeo ya
awali ya uchaguzi wa serikali za mitaa Desemba 14,2014, wilayani Ngara mkoani
Kagera yanaonesha kuwa Chama cha Mapinduzi kinaongoza kikifuatiwa na Chadema
huku Chama cha NCCR Mageuzi kikifuatia .
Kaimu Msimamizi
wa uchaguzi wilaya ya Ngara Bw Fred Kakuru amesema hadi kufikia jana Desemba
16,2014, katika vijiji vilivyopiga kura 69, Chama cha Mapinduzi kimeshinda
vijiji 61, Chadema vijiji vitatu huku NCCR Mageuzi kikipata kijiji kimoja.
Amesema
vitongoji 338 vilivyofanya uchaguzi kati ya vitongoji 394 vilivyopo, Chama cha
Mapinduzi kimeshinda vitongoiji 294, Chadema vitongoji 43 na NCCR Mageuzi
kitongoji kimoja.
Bw Kakuru
amesema vijiji vingine vitatu vyenye vitongoji 8 vimefanya uchaguzi leo Desemba
17,2014 na kwamba kijiji cha Mbuba kitafanya uchaguzi Jumapili kutokana na
vifaa vilivyotakiwa kupelekwa kwenye kijiji hicho, vilipelekwa sehemu nyingine
KIBONDO.
Msimamizi wa
uchaguzi katika Halmashauri ya Wilaya ya Kibondo Bw Judethadius Mboya
amebatilisha matokeo ya uchaguzi kwa wenyeviti wa vitongoji 28 baada ya kubaini
kasoro katika vituo hivyo na ukiukwaji wa sheria za uchaguzi.
Bw Mboya
amezitaja sababu za kubatilisha matokeo hayo kuwa ni kuongezeka kwa idadi ya
wapiga kura tofauti na waliojiandikisha, dosari kwenye karatasi za kupigia kura
kwa kubadili majina ya wagombea pamoja na wagombea kulingana kura.
Amesema
vituo hivyo 28 vinatarajia kufanya uchanguzi baada ya siku 7 kuanzia sasa ili
kutoa fursa kwa wananchi kuchangua upya viongozi wao kulingana na kanuni,
taratibu na sheria za uchaguzi.
Bw Mboya
amewataka wakazi wa maeneo ambayo uchaguzi wao umesogezwa mbele kuwa na subira
kwa kuwa imefanyika hivyo kwa nia njema.
Habari
Na:-Radio kwizera FM-Ngara.
|
No comments:
Post a Comment