Bunge
nchini Kenya.
Bunge
lililazimika kuahirisha vikao vyake kwa dakika 30 kufuatia mtafaruku huo.
Kikao cha
leo kilikuwa kikao maalum ambacho kilipaswa kupitisha muswada huo ambao baadaye
utaidhinishwa na Rais Kenyatta kuwa sheria.
Wabunge wa upinzani waliupinga muswada huo na kuanza kurusha karatasi sakafuni
huku wakitatiza shughuli bungeni humo.
Mwenyekiti
wa Kamati ya Usalama wa Bunge, Bwana Asman Kamama, alijaribu kutaja mabadiliko
yaliyopendekezwa kufanyiwa muswada huo lakini wabunge walianza kuimba na
kumzomea spika wa bunge wakiukataa muswada huo wakisema 'bado mapambano.'
Spika wa
Bunge hilo, Justin Muturi kuna kipindi alimuru walinzi wa bunge kuwaondoa
baadhi ya viongozi waliofika bungeni humo kwa mjadala ambao ulitarajiwa kuwaka
moto, hasa wa upande wa upinzani.
Mswada huo
ambao umewasilishwa bungeni kufuatia matukio ya ukosefu wa usalama na
mashambulizi nchini Kenya, unapendekeza kuwa washukiwa wa ugaidi wanaweza
kuzuiliwa kwa mwaka mmoja huku polisi wakifanya uchunguzi.
Mapendekezo
ya muswada huo ni kwamba mshukiwa wa ugaidi anaweza kuzuiliwa kwa siku 360
kutoka siku 90 za awali.
Pia ikiwa
muswada huo utapitishwa kuwa sheria, mashirika ya habari yatatozwa faini ya
hadi shilingi milioni 5 kwa kuchapisha taarifa au picha ambazo zinaleta hofu na
kusababisha taharuki.
Muswada huu
umetolewa kufuatia mashambulizi yaliyofanywa na wapiganaji wa Al Shabaab
wanaowataka wanajeshi wa Kenya kuondolewa Somalia.
Rais
Kenyatta amekuwa akikabiliwa na shinikizo la kuimarisha usalama wa tangu
mashambulizi ya Septemba mwaka 2013 katika jengo la maduka ya kifahari la
Westgate mjini Nairobi ambapo watu 67 waliuawa.
|
No comments:
Post a Comment