AFYA YETU:-Ampicillin; Dawa za kutibu U.T.I (2)Usizitumie sanjari na dawa za kupanga uzazi. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Monday, December 22, 2014

AFYA YETU:-Ampicillin; Dawa za kutibu U.T.I (2)Usizitumie sanjari na dawa za kupanga uzazi.

Mpendwa msomaji nakushukuru kwa kutenga muda wako kwa ajili ya kusoma safu hii. Katika makala yetu ya leo nitaendelea kutoa maelezo ya namna bora ya kutumia dawa za kutibu U.T.I. Kwa faida ya wasomaji wapya nitaelezeza tena kwa ufupi kuhusu ugonjwa wa U.T.I.

U.T.I ni kifupi cha (Urinary tract Infection) ni ugonjwa unaoathiri njia ya mkojo. Ugonjwa huu husababisha maumivu makali mwilini. Baadhi ya dalili za ugonjwa huu ni pamoja na mwili kuwa dhaifu, kujisikia kichefuchefu mara kwa mara, mkojo kuwa wa moto na mchafu, maumivu wakati wa kukojoa, maumivu kwenye kiuno na tumbo kuuma.

Ugonjwa huu hutokea pale mlango wa njia ya haja ndogo inaposhambuliwa na bacteria. Bakteria hawa wasipotibiwa mapema huenea hadi kwenye figo na athari zake zinaweza kuwa mbaya zaidi.

Uganjwa huu hutibika kwa dawa nyingi jamii ya vijiua sumu (antibiotic). Baadhi ya dawa hizi ni tetracycline, ampicillin, Ciprofloxacin, Cefalexin, Cefadroxil, clavam, Fosfomycin, Monurol, Furadantin, Sulfam ethoxazole, co-trimax, ampicillin, gentamicinn na nyinginezo.

Wiki iliyopita nilieleza namna ya kutumia dawa tetracycline katika kutibu U.T.I. 

Katika makala yetu ya leo nitaeleza nammna ya kutumia ampicillin kutibu U.T.I. 

Ampicillin ni moja ya dawa jamii ya vijiuasumu (antibiotics) inayotumika kutibu magonjwa yanayoambukizwa na bakteria ikiwemo U.T.I. Dawa hii hutibu U.T.I kwa kuingilia ukuaji wa bakteria walioko mwilini kwa kuua seli zake wakati wanakuwa. 

Hali hii husababisha seli za bakteria kuwa dhaifu, hatimaye kufa.

Ampicillin ni jina la jumla la dawa hii na imesajiliwa. Inatumika Tanzania kwa majina tofauti ya kibiashara. Baadhi ya majina haya ni Omnipen, Polycillin na Principen.

Taarifa muhimu kabla ya kutumia ampicillin:

Baada ya kufanyiwa vipimo na kubainika kuwa una U.T.I unatakiwa kujadiliana na daktari kuhusu dawa atakazokupatia. Kuwa huru na muwazi kumweleza daktari kuhusu mstakabali wa afya yako.

Mweleze daktari au mfamsia au muuguzi kama una ujauzizo au unapanga kupata ujauzito wakati ukitumia ampicilini au unanyonyesha. 

Baadhi ya dawa katika kundi la vijiuasumu haziruhusiwi kwa kuwa zinaweza kuwa na madhara kwa mtoto aliyeko tumboni. 

Hata hivyo ampicillin inaweza kutumia. Kumbuka kutokutomia dawa pasipo maelekezo ya daktari hasa wakati wa ujamzito au kunyonyesha. Pia mweleze daktari, mfamasia au muuguzi kama unatumia dawa nyingine za tiba au vyakula nyongeza (food supplement), huwa unapata mzio ukitumia baadhi ya dawa au vyakula na una matatizo ya tumbo au kuharisha. Taarifa hizi zitakusaidia wewe kuandikiwa dawa zitakazokufaa kulingana na hali yako ya kiafya.

Baadhi ya dawa za tiba haziwezi kufanya kazi sanjari na dawa nyingine. Ampicillin pia zina tabia hii. 

Mweleze daktari kama unatumia dawa yoyote kabla hajakuandikia dawa. Baadhi ya dawa ambazo hazitumiwi sanjari na ampicillini ni tetracycline hasa doxycline. Dawa hii huingilia utendaji kazi wa ampicillin mwilini na kuifanya kukosa ufanisi. 

Dawa nyingine ambazo hazipaswi kutumika sambamba na ampicillin ni Probenecid, Allopurinol, Anticoagulants (heparin, warfarin) au methotrexate na Aminoglycosides (mfano; gentamicin. Probenecid huongeza madhara kwa mgonjwa kama tutakavyoona baadaye na Allopurinol inaweza kuongeza vipele kwenye mwili.
 
Kwa upande wa Anticoagulants hasa heparin, warfarin au methotrexate, haishauriwi kwa kuwa ampicillin inaweza kumwongezea madhara mgonjwa. Haya ni madhara ambayo kila anayetumia dawa huyapata na yanavumilika.

Dawa za Aminoglycosides hasa gentamicin na za kupanga uzazi hazitumiki sanjari na ampicillin kwa kuwa zinaweza kupunguzwa nguvu ya utendaji kazi wake mwilini.

Zinaweza kuwepo dawa nyingine zisizopaswa kutumika sanjari na ampicillin, unachoshauriwa kufanya ni kumweleza daktari kama unatumia dawa nyingine za tiba.

MATUMIZI SAHIHI YA DAWA

Tumia ampicillin kama ulivyoelekezwa na daktari. Itumie kwa kiasi, muda na wakati, kadri ulivyoelekezwa na daktari. Usiongeze wala kupunguza kiasi cha dawa na muda wa kuzitumia, ili kuepusha madhara. Maelezo juu ya kifungashio cha dawa hii yatakusaidia kutumia ampicillin kwa usahihi.

Tumia ampicillin kwa kunywa angalau nusu saa kabla ya kula au saa mbili baada ya kula. Kunywa maji ya kutosha, kadri daktari atakavyokuelekeza, wakati unatumia dawa hii.

Ili uweze kupata nafuu au kupona kabisa tumia dozi nzima ya ampicillin. Usikatishe dozi hata kama utajisikia kupona.

Ikitokea umesahau kutumia dawa, tumia mara moja mara baada ya kukumbuka. Kama umekumbuka wakati wa kutumia dawa umekaribia, usitumie dawa, subiri dozi inayofuata na kisha urejee katika utaratibu wako wa awali.

TAHADHARI

Usiitumie kutibu magonjwa yanayoambukizwa na virusi kama vile baridi.

Imeandaliwa na Martin Malima kwa msaada wa mitandao.

UNGANANASI KATIKA  FACEBOOK , TWITTER , INSTAGRAM , Pia tutumie tukio la Picha kwa WhatsApp +255789925630.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad