MUENDELEZO WA MWANAMKE KUJICHOMA KISU KIFUANI:- Chanzo chahisiwa ni Matatizo ya Kiakili na Amelazwa katika chumba cha Wagonjwa Mahututi namba 4 Hospitali ya Murgwanza-Ngara. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Monday, July 14, 2014

MUENDELEZO WA MWANAMKE KUJICHOMA KISU KIFUANI:- Chanzo chahisiwa ni Matatizo ya Kiakili na Amelazwa katika chumba cha Wagonjwa Mahututi namba 4 Hospitali ya Murgwanza-Ngara.

Mwanamke huyu amejulikana kwa jina la Prisca Joshua  mkazi wa Nakatunga ,Mamlaka ya Mji mdogo wa Ngara mkoani Kagera,  amenusurika kifo baada ya kujichoma kisu  jana Julai 13,2014,Majira ya saa za Jioni,  sehemu ya chini ya kifua  akiwa nyumbani kwake  huku Chanzo cha kujichoma kikidhaniwa kuwa ni Kutokana na matatizo ya akili..(Picha hii na Maktaba yetu).

Akizungumza na Radio Kwizera,  Daktari  katika hospitali ya Murgwanza  Dr Mbise Willison ambaye ndiye aliyempokea mwanamke  huyo amesema amempokea jana majira ya saa 2 usiku huku akiwa anavuja damu  na kisu alichojichoma kikiwa bado  kimenasa katika sehemu ya chini ya kifua ambapo ndipo alijichoma.

Amesema baada ya  kumpokea  mgonjwa huyo walifanikisha kukiondoa kisu hicho  na kugundua kuwa kimeathili sehemu ya  Ini  na damu zilivujia kwa ndani   na kusema kuwa  damu hizo walifanikisha kuziondoa na hali ya mgonjwa inaendelea vizuri ikilinganishwa na ilivyokuwa jana kipindi analetwa hospitalini hapo.

Kwa upande wake Dada yake ,Bi Jiliani Joshua ambaye  anamuuguza  mwanamke huyo amesema kuwa mdogo wake anashi na mwanaye mmoja  na haishi na mumewe  na katika kufanya tukio hilo alijifungia chumbani  kwake  na kufungulia muziki  mkubwa na hivyo kujichoma kisu hicho na ndipo majirani walifika kumuokoa na kufanikiwa  kumfikisha hospitali na kwamba taarifa za tukio hilo alizipata kupitia kwa majirani kwani yeye anashi mbali na yeye.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad