KESI YA MBASHA:-Imesomwa tena Julai 17,2014 na hiki ndicho kilichoamuliwa na Mahakama… - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Friday, July 18, 2014

KESI YA MBASHA:-Imesomwa tena Julai 17,2014 na hiki ndicho kilichoamuliwa na Mahakama…


Mume wa mwimbaji wa nyimbo za injili nchini Frola Mbasha,Mr.Emanuel Mbasha Jana (Al Hamis Julai 17,2014) amepandishwa tena kizimbani katika Mahakama ya Wilaya ya Ilala,Jijini Dar es Salaam kujibu mashtaka mawili yanayo mkabili ya ubakaji.

Katika kesi hiyo inayoendeshwa na Hakimu Wilbert Luago,amelazimika kuhairisha kesi hiyo kwa muda wa nusu saa kwa hoja aliyoitoa Mbasha kwamba ana wakili wa kumtetea lakini alishindwa kufika kutokana na matatizo ya usafiri.

Kauli hiyo ya Mbasha ilimfanya Hakimu Luago kuhoji kama kweli alikuwa na nia ya kuwa na wakili au ana nia ya kuweka wakili kwani tangu kesi hiyo imeanza Mbasha hajapeleka wakili yoyote.

Mara baada ya nusu saa kupita Wakili wa mshitakiwa alituma muakilishi wake kuwakilisha barua za dharula ambazo zilionesha kuwa yupo safarini mkoani Arusha na kuomba kesi hiyo kuahirishwa.

Emanuel Mbasha ana kabiliwa na kesi mbili za ubakaji ambapo inadaiwa alitenda makosa hayo maeneo ya Tabata katika nyakati mbili tofauti,Mbasha alisindikizwa mahakamani na ndugu zake huku Mkewe Flora Mbasha kutoonekana Mahakamani na badala yake alionekana mdogo wake Flora ambaye ni shemeji yake Emanuel Mbasha.
Kesi hii imehairishwa mpaka July 23 mwaka huu.




No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad