Evans Elieza
Aveva ameshinda Urais wa Klabu ya Simba katika Uchaguzi mkuu wa klabu hiyo June
29, 2014 chini ya Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi,Wakili,Dk Damas Ndumbaro.
|
Geofrey
Nyange ‘Kaburu’ amepata kura 1043, amefuatiwa na Jamhuri Kihwelo ‘Julio’, kura
413 na mwisho Sued Nkwabi 300.
|
Evans Aveva
amechaguliwa kuwa Rais mpya wa Klabu ya soka ya Simba katika uchaguzi mkuu
uliofanyika jana (June 29,2014) kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Bwalo la Polisi,
Oysterbay jijini Dar es Salaam.
Aveva
alipata ushindi huo wa kimbunga baada ya kupata kura 1845 na kumgaragaza
mpinzani wake Andrew Tupa aliyepata kura 387 huku kura sita zikiharibika.
Katika
nafasi ya Makamu wa Rais, Geofrey Nyange ‘Kaburu’ ameshinda nafasi hiyo baada
ya kupata kura 1043 huku Jamhuri Kihwelo ‘Julio’ akipata kura 413 na Swedy
Mkwabi akipata kura 300.
Awali,
aliyekuwa mgombea Urais wa klabu hiyo, Michael Wambura alizuiwa na Kamati ya
Uchaguzi ya Simba kuingia kwenye Ukumbi.
Wambura,
alienguliwa kwa kuwa amesimamishwa uanachama na baadaye kwa kukiuka taratibu za
uchaguzi, alishindwa kupiga kura kutokana na uamuzi wa kumzuia kuingia
ukumbini.
Kwa mujibu
wa wasimamizi waliokuwa wakihakiki uhalali wa wanachama kwenye uchaguzi huo,
jina la Wambura halikuwapo katika orodha ya wanachama wanaostahili kupiga kura.
Wambura kama
walivyokuwa wanachama wengine, walifika katika eneo la uchaguzi kwa ajili ya
kukamilisha haki hiyo ya kikatiba, lakini alionekana kushangazwa na uamuzi huo
wa kuzuiwa kupiga kura.
No comments:
Post a Comment